Skip to main content

BAADA YA KUONA MAMBO MAGUMU KWA WAARABU…ADEBAYOR AANZA KUJISOGEZA SIMBA KIAINA…

BAADA YA KUONA MAMBO MAGUMU KWA WAARABU…ADEBAYOR AANZA KUJISOGEZA SIMBA KIAINA… | Soka La Bongo

Kiungo Mshambuliaji kutoka nchini Niger na Klabu ya RS Berkane ya Morocco Victorien Adebayor amesema anatarajia siku moja atacheza Simba SC, kufuatia kuvutiwa na utamaduni wa Klabu hiyo ya Msimbazi, Dar es salaam.

Adebayo alikaribia kutua Simba SC wakati wa Usajili wa Mwanzoni mwa msimu huu, lakini RS Berkane iliizidi kete Klabu hiyo ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kumwaga fedha nyingi za usajili, wakimtoa USGN ya Niger.

Akizungumza kutoka nchini Morocco Adebayor amesema, bado anatamani kucheza Simba SC katika maisha yake, kwa sababu anajua klabu hiyo ina mambo mengi ambayo anaendana nayo, hususan mapenzi alioonyeshwa na Mashabiki alipotua Dar es salaam kwa mchezo wa Hatua ya Makundi Kombe la Shirikisho Barani Afrika msimu uliopita.

“Nilitamani kucheza Simba SC, ni Klabu ambayo ilionyesha kila hatua ya kunihitaji, hasa mashabiki wao nawakumbuka sana upendo walionionesha nikiwa hapo Tanzania”

“Wakati ule kulikuwa na ugumu kwa Simba SC walitakiwa kukamilisha dili lile huku wakishindana na Klabu nyingine iliyohitaji huduma yangu, kwa hiyo ilikua ngumu sana.”

“Bado ninaikumbuka Simba SC nawakumbuka sana Mashabiki wake, naamini utakuja wakati ninaweza kuja kuichezea Simba SC hivi karibuni.” amesema Adebayor

Tangu alipojiunga na RS Berkane mwanzoni mwa msimu huu, Adebayor amekua na wakati mgumu wa kucheza mara kwa mara katika kikosi cha kwanza cha klabu hiyo, kama ilivyokua USGN ambapo alitegemewa sana katika safu ya ushambuliaji.

The post BAADA YA KUONA MAMBO MAGUMU KWA WAARABU…ADEBAYOR AANZA KUJISOGEZA SIMBA KIAINA… appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/plQSCet

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT