Skip to main content

Aziz Ki & Chama… Watibua Mipango Baada ya Kukipata Walichokuwa Wanakitaka



Aziz Ki & Chama… Watibua Mipango Baada ya Kukipata Walichokuwa Wanakitaka

Stephane Aziz Ki na Clatous Chama.

MCHUMA janga hula na wakwao. Itakuwa hivyo kwa mastaa wawili wa Yanga na Simba ambao wamekipata walichokuwa wanakitaka.

Mashabiki watakosa kuona zile burudani zao kwenye mechi tatu kutokana na makosa ambayo waliyafanya jambo ambalo limetibua mipango ya benchi la ufundi kwa timu hizo.

Stephane Aziz Ki na Clatous Chama, watakosekana kwenye dakika 270 ambazo ni mechi tatu, baada ya kufungiwa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) kwa kosa la kukwepa kusalimiana.

Hayo yalifanyika kwenye Kariakoo Dabi iliyochezwa Uwanja wa Mkapa, Oktoba 23, mwaka huu na ubao ukasoma Yanga 1-1 Simba.

Katika mchezo huo wa Ligi Kuu Bara, bao la Yanga alifunga Aziz Ki kwa pigo la faulo, huku kwa upande wa Simba, Chama alimpa pasi Augustine Okrah, akafunga bao.

Mbali na mastaa hao kukosekana kwenye dakika hizo 270, wametozwa faini ya shilingi laki tano kila mmoja kwa kosa hilo.

Hapa Spoti Xtra linakuletea mipango iliyotibuliwa na nyota hao msimu huu.

MAPIGO HURU

Nyota hawa kazi yao kubwa kwenye timu zao ilikuwa ni kwenye upigaji wa mapigo huru, hivyo kukosekana kwao kutalifanya benchi la ufundi kuwatumia nyota wengine.

Aziz Ki na Chama wote wametupia kutokana na mapigo huru. Aziz Ki alifunga kwa faulo dhidi ya Simba, huku Chama akifunga kwa pigo la penalti dhidi ya Geita Gold.

Aziz Ki kwenye mchezo dhidi ya Polisi Tanzania alipiga jumla ya kona 8, alipiga faulo 4 sawa na zile alizopiga mchezo dhidi ya Coastal Union.

Chama kwenye mchezo dhidi ya Geita Gold alipiga faulo tatu na penalti moja, mchezo dhidi ya Prisons alipiga faulo tano na kona moja, hivyo kukosekana kwao kumetibua mipango ya benchi la ufundi.

HAPA WALIWATIBULIA WAPINZANI

Wakati Simba ikipambana kutibua rekodi ya Yanga kucheza mechi bila kufungwa na Yanga wakihitaji kuitungua Simba, mpango ulianza kuonekana kujibu kwa Msimbazi dakika ya 13 kupitia kwa Agustine Okrah aliyefunga bao kwa pasi ya Chama.

Kabla hawajaenda mapumziko, Aziz Ki alitibua mipango kwa kufunga bao lililotibua furaha ya Wanasimba, hivyo kwenye mchezo huo wa dabi uliochezwa Uwanja wa Mkapa Oktoba 23 kila mmoja alitibua mipango ya wapinzani wake.

PASI ZA MWISHO

Ile vita yao ya kuwatengenezea washambuliaji wao mabao sasa imetibuliwa kwa dakika 270 ambapo Aziz Ki ana pasi moja ya bao na Chama anazo tatu.

Mipango yao imetibuliwa na itawabidi wasubiri mpaka watakaporejea uwanjani kurejesha makali yao.

DAKIKA ZAO KUGANDA

Hakutakuwa na mwendelezo wa dakika zao za kutumika uwanjani kwa kuwa watakuwa jukwaani mpaka watakaporejea wataendelea kuongeza mwendo kwenye dakika zao.

Aziz Ki ni mechi 7 kacheza akiwa ameyeyusha dakika 468, katupia mabao mawili na pasi moja ya bao.

Chama alikuwa ameyeyusha dakika 712 baada ya kucheza mechi 8 akitupia bao moja na pasi tatu za mabao.

KETE TATU ZA CHAMA

Singida Big Stars (Novemba 9)

Ihefu (Novemba 12)

Namungo (Novemba 16)

KETE TATU ZA AZIZ KI

Kagera Sugar (Novemba 13)

Singida Big Stars (Novemba 17)

Dodoma Jiji (Novemba 22)

Juma Mgunda, Kocha Mkuu wa Simba, alisema kukosekana kwa Chama kunatibua mipango ya timu hiyo kutokana na umuhimu wa kila mchezaji kwenye kikosi chake.

“Kama una mtoto akaguswa jichoni akaumizwa unadhani utapenda? Haiwezi kuwa hivyo, Chama ni mchezaji wa Simba, anapaswa kutimiza majukumu ya Simba, kukosekana kwake maana yake kuna mipango itavurugika, lakini wapo wachezaji wengine watacheza,” anasema Mgunda.

Kwa upande wa Nasreddine Nabi, Kocha Mkuu wa Yanga, hivi karibuni alisema kuwa kila mchezaji anapokosekana kwenye kikosi humlazimu kubadili mpango kazi.

“Anapokosekana mchezaji mmoja ambaye huwa anaanza kwenye timu kinachofanyika ni kubadili mpango kazi kwenye mechi husika,” anasema Nabi.

Aziz Kin a Chama kila mmoja amefungiwa mechi tatu za Ligi Kuu Bara na faini ya shilingi laki tano.

Aziz Ki amefunga mabao mawili kwenye Ligi Kuu Bara msimu huu.

Chama msimu huu kwenye ligi amehusika katika mabao manne, akifunga moja na asisti tatu.







Toa comment

The post Aziz Ki & Chama… Watibua Mipango Baada ya Kukipata Walichokuwa Wanakitaka appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/OBHUz0J

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT