Skip to main content

Afrika CDC yataka mifumo thabiti ya afya ya jamii kukabiliana na mzigo wa magonjwa Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Maradhi cha Af…

Afrika CDC yataka mifumo thabiti ya afya ya jamii kukabiliana na mzigo wa magonjwa

Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Maradhi cha Afrika (Africa CDC), kimetoa wito wa kuundwa kwa kundi la wafanyakazi wa afya ya jamii wanaofadhiliwa vya kutosha, waliofunzwa na kuhamasishwa ili kuzisaidia nchi za Afrika kukabiliana na mzigo unaoongezeka wa magonjwa.
Ofisa mwandamizi wa Africa CDC Bibi Herilinda Temba amesema hayo kwenye warsha iliyofanyika mjini Mombasa, na kusisitiza kuwa uwekezaji katika mfumo thabiti wa afya ya jamii utaongeza uwezo wa bara la kutabiri, kutambua na kutibu magonjwa.
Bibi Temba pia amesema kuajiri wafanyakazi wa ziada wa afya ya jamii pia kutaongeza ufufukaji baada ya janga la UVIKO-19 barani Afrika, ikiashiria kuwa wahudumu wa afya katika jamii wamekuwa wahusika muhimu katika kuongeza uelewa wa kupambana na magonjwa ya kuambukiza kama vile kifua kikuu na VVU/UKIMWI pamoja na kuwasaidia wagonjwa kufuata matumizi ya dawa za muda mrefu.

The post Afrika CDC yataka mifumo thabiti ya afya ya jamii kukabiliana na mzigo wa magonjwa Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Maradhi cha Af… appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/63751/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT