Skip to main content

22 kuiwakilisha Tanzania michezo ya wenye walemavu wa akili duniani

Na Norah Damian, Mtanzania Digital

Wachezaji 22 wenye ulemavu wa akili wanatarajia kuiwakilisha Tanzania kwenye michezo ya Dunia inayotarajia kuanza Mei 13 hadi Juni 12, 2023 Berlin Ujerumani.

Katika mashindano hayo Tanzania itawakilishwa na michezo miwili ambayo ni riadha na mpira wa wavu.

Washiriki hao walipatikana kupitia mashindano ya Taifa yaliyofanyika jijini Mwanza Desemba 2021 ambapo mchezo wa riadha ulifanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba wakati wa soka na mpira wa wavu ilichezwa kwenye viwanja vya Sekondari ya Wavulana Bwiru.

Akizungumza na Mtanzania Digital, Mkurugenzi wa Olimpiki Maalumu Tanzania, Charles Rays, amesema msafara huo pia utajumuisha makocha na wazazi wa watoto hao.

Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, baadhi ya wachezaji watakaoiwakilisha Tanzania kwenye mashindano hayo ni Sheha Haji, Abdulrahman Shabani, Julius Francis, Uwesu Salim, Ally Nassor Juma, Duncan Anaclet, Emmanuel Chano na Mathias Makanyaga.

Wengine ni Fatuma Hashim, Maimuna Juma Ally, Judith Mbila na Nzobinimana Claudine.

Aidha amesema ili kufanikisha ushiriki wa mashindano hayo ya Dunia zinahitajika Sh milioni 195.

Mwaka 2019 mashindano hayo yalifanyila Abu Dhabi Dubai na kushirikisha nchi 183 ambapo Tanzania iliwakilishwa na timu mbili za riadha na wavu. Mmoja wa wachezaji, Khalifani Ally Jihadi alishiriki mbio za mita 200 na kufanikiwa kushinda medali ya dhahabu.

The post 22 kuiwakilisha Tanzania michezo ya wenye walemavu wa akili duniani appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/63561/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT