Skip to main content

YANGA WAJA NA MBINU MPYA

BAADA ya ubao wa Uwanja wa Mkapa kusoma Yanga 1-1 Al Hilal mastaa wa Yanga wamerejea kambini na kuanza mazoezi kwa ajili ya mchezo wao wa marudio.

Mpango mpya kwa sasa ni kuwarejesha mastaa wote kwenye ubora wao na kufanyia kazi makosa ambayo walifanya mchezo uliopita Oktoba 8,2022.

Jumapili ya Oktoba 16,2022 mchezo huo unatarajiwa kuchezwa nchini Sudan ambapo mshindi wa jumla atafuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.

Saa 3:00 usiku mchezo huo ambao utakuwa na ushindani mkubwa unatarajiwa kuchezwa na tayari mikakati inapangwa kuelekea mchezo huo.

Miongoni mwa nyota ambao wameanza mazoezi ni pamoja na kiungo mshambuliaji Bernard Morrison, Dickson Ambundo, Heritier Makambo na Fiston Mayele.

Nasreddine Nabi, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo ujao na wana imani ya kupata ushindi.

“Kupata sare kwenye mchezo wa kwanza haina maana kwamba kazi imekwisha, bado tuna nafasi ya kufanya vizuri mchezo wetu ujao na kutimiza malengo.

“Hakuna ambaye anaamini kwamba mchezo utakuwa mwepesi hilo lipo wazi lakini tunafanya kila kitu kiwe sawa ili tupate ushindi,”.

The post YANGA WAJA NA MBINU MPYA appeared first on Saleh Jembe.

The post YANGA WAJA NA MBINU MPYA appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/2Z6xsbg

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT