Skip to main content

Wabunifu Chipukizi 15 kuwania tuzoya Emering Designer

Na Jeremia Ernest, Mtanzania Digital

WABUNIFU chipukizi 15, wameingia katika king’anyiro cha kuwania tuzo ya Emering Designer, inayotolewa kila mwaka katika tamasha la Swahili Fashion Week.

Tuzo hiyo ambayo ilipewa jina la aliyekuwa Mratibu wa Jukwaa hilo marehemu Washington Benbella, ni mahususi kwa wabunifu chipukizi inawapa nafasi ya kushindanisha kazi zao bure katika jukwaa hilo.

Akizungumza na Mtanzania Digital leo, muasisi wa tamasha hilo Mustapha Hasanali, amesema maombi yalikuwa mengi kumefanyika mchujo na majaji wazoefu wakiongozwa na chifu jaji Jamila Veraswai mpaka kupata wabunifu 15.

“Tulitoa fursa kwa wabunifu kujisajili kuwania tuzo hii hatimae walio pita ni 15 ambapo wabunifu wa tatu wanatoka nchi za jirani ambazo ni Lubumbashi DRC, Nairobi Kenya na Terni Italy,” amesema Mustapha Hasanali.

Ameongeza kuwa wengine wametoka Tanzania katika mikoa mbalimbali ikiwemo Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Shinyanga, Pwani na Dodoma.

Huu ni msimu wa 15 wa tamasha la Swahili Fashion Week ambalo litafanyika kuanzia Desemba 2 mpaka 4 jijini Dar es Salaam.

The post Wabunifu Chipukizi 15 kuwania tuzoya Emering Designer appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/RXL63uz

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT