Skip to main content

TIKETI 10,000 MASHABIKI WA YANGA KUPEWA KUWAONA WAARABU

UONGOZI wa Yanga umetangaza kugawa bure tiketi 10,000 za mchezo wa Yanga dhidi ya Club Africain ya nchini Tunisia kwa mashabiki watakaochanja chanjo ya Uviko-19.

Yanga wanatarajiwa kukutana na Club Africain Novemba 2 katika mchezo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho Afrika kuwania kufuzu hatua ya makundi ya michuano hiyo, kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.

 CEO wa Yanga, Andre Mtine, amesema kuwa katika kuhakikisha kuwa wanaendelea kutoa elimu juu ya magonjwa ya Uviko-19, watatoa chanjo kwa mashabiki 10,000 ambao watachanjwa, hivyo jambo hilo kwao wanafanya kama sehemu ya kuelimisha jamii.

“Ushirika wetu na UNICEF kuhusu Uviko-19 na virusi vya Ebola umeanza kazi rasmi ambapo tunatoa zawadi ya tiketi 10,000 kwa mashabiki ambao watachanja chanjo ya Uviko-19 kushuhudia mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Club Africain utakaochezwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa tarehe 2 mwezi ujao,” amesema.

Kwa upande wa Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe amesema:“Kila mmoja wetu anafahamu madhara ya Uviko-19, hivyo kupambana na Uviko-19 ni jukumu letu sote. Sisi kama Klabu tunatamani mitaa iwe salama.

“Hatuwezi kutoa burudani kama hatutoi elimu ya afya. Tumeandaa vitu mbalimbali, na utakutana na viongozi mbalimbali wa klabu yetu ambao watakuja kutoa hamasa. Mayele, Feisal na Aziz Ki pamoja na wachezaji wengine watakuwepo mitaani kutoa elimu hiyo na kuhamasisha” amesema Kamwe.

The post TIKETI 10,000 MASHABIKI WA YANGA KUPEWA KUWAONA WAARABU appeared first on Saleh Jembe.

The post TIKETI 10,000 MASHABIKI WA YANGA KUPEWA KUWAONA WAARABU appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/t9xUIOZ

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT