Ten Hag Aaahidi Kumalizana na Ronaldo Baada ya Kuonesha Utovu wa Nidhamu
Cristiano Ronaldo
KOCHA wa Manchester United Erik Ten Hag amesema atamalizana na mchezaji wake Cristiano Ronaldo baada ya kuonesha kitendo cha utovu wa nidhamu katika pambano dhidi ya Totenham Hotspurs lililomalizika kwa Manchester United kushinda kwa mabao 2-0.
Katika mchezo huo Ronaldo alionekana kuondoka uwanjani na Kwenda kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ikiwa ni dakika 10 kabla ya mchezo kumalizika ikiwa ni ishara ya kuonesha kutoridhishwa na kukaa benchi.
Akijibu swali kwa mwandishi wa Habari wa Amazon Prime, Ten Hag alinukuliwa akisema:
“Alikuwepo pale, nilimuona lakini sikuongea naye.”
Erik Tem Hag
Huwa sitilii maanani vitu kama hivyo, ntalifanyia kazi hilo suala kesho (leo), nataka kila kitu kielekezwe kwenye timu.
Ronaldo amekuwa na tabia ya kutawala vichwa vya Habari vya mitandao ya kijamii pamoja na vyombo vya Habari kutokana na kuwa na baadhi ya matukio ambayo yanaonesha utovu wa nidhamu hasa nje ya uwanja kutokana na ukubwa wa jina lake.
Toa comment
The post Ten Hag Aaahidi Kumalizana na Ronaldo Baada ya Kuonesha Utovu wa Nidhamu appeared first on soka letu.
source https://mjombazecoder.website/57996/





Comments
Post a Comment