Skip to main content

SIMBA YAPIGA 5G, MTIBWA MAJANGA KADI NYEKUNDU ZAWAPONZA

KIUNGO wa kazi ngumu ndani ya kikosi cha Simba, Mzamiru Yassin amerejea na nyota kali kwa kuwa miongoni mwa waliofunga mabao kwenye mchezo wa leo dhidi ya Mtibwa Sugar.

Baada ya dakika 90 kukamilika, ubao wa Uwanja wa Mkapa umesoma Simba 5-0 Mtibwa Sugar na kuifanya Simba kusepa mazima na pointi tatu.

Mzamiru alifungua pazia la mabao dakika ya 38 kisha mabao mawili yalifungwa na Pape Sakho dakika ya 48 na 90 huku Okra akifunga bao moja dakika ya 63 na Moses Phiri naye alitupia bao moja na kufikisha mabao matano.

Ilikuwa siku mbaya kwa Mtibwa Sugar kwa wachezaji wawili kuonyeshwa kadi nyekundu alianza Pascal Kitenge kish nahodha Issa Rashid.

Huu ni ushindi wa kwanza mkubwa kwa Simba chini ya Kocha Mkuu Juma Mgunda ndani ya ligi ambaye alitoka kupoteza kwa kufungwa bao 1-0dhidi ya Azam FC.

Salum Mayanga, Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar amesema kadi mbili nyekundu zimewavurugia mipango ya kusaka ushindi pamoja na kuumia kwa kipa namba moja Faroukh Shikalo.

The post SIMBA YAPIGA 5G, MTIBWA MAJANGA KADI NYEKUNDU ZAWAPONZA appeared first on Saleh Jembe.

The post SIMBA YAPIGA 5G, MTIBWA MAJANGA KADI NYEKUNDU ZAWAPONZA appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/58711/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT