Skip to main content

Simba Yaonja Uchungu wa Mwiko, Yapigwa na Azam Uwanja wa Mkapa




Simba Yaonja Uchungu wa Mwiko, Yapigwa na Azam Uwanja wa Mkapa

SIMBA chini ya kocha mkuu wa muda, Juma Mgunda, ilikuwa imejipa mwiko kuwa haitapoteza mechi yoyote msimu huu kirahisi, lakini jana Azam FC wamevunja mwiko huo.

Katika mchezo huo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, Simba ilikumbana na kipigo cha bao 1-0 na kubaki nyuma kwa tofauti ya pointi tatu dhidi ya mabingwa watetezi Yanga wanaokamata nafasi ya kwanza.

Simba ilikuwa na majeruhi kibao kuelekea mchezo huo ambapo Sadio Kanoute hakuwepo pamoja na Mzamiru Yassin, Shomari Kapombe ambao kutokana na matatizo ya majeraha na kadi waliikosa mechi hiyo.

Bao pekee la Azam FC katika mchezo huo lilifungwa na Prince Dube dakika ya 34 akitumia vizuri makosa ya safu ya ulinzi ya Simba kuiadhibu Simba nzima.

Habib Kyombo atajilaumu mwenyewe kwa kukosa nafasi mbili za wazi dakika ya 13 na 44 katika mchezo huo.

Matokeo hayo yanaifanya Simba ibaki na pointi 14 katika nafasi ya tatu huku Mtibwa wakiwa juu yao wakiwa na alama 15 lakini wakiwa wamecheza michezo miwili zaidi.

Yanga ni vinara wa msimamo wakiwa na pointi 17 baada ya kucheza michezo saba huku Simba wakiwa na pointi 14 baada ya michezo hiyo saba.

Huu ni mchezo wa kwanza kocha Juma Mgunda anapoteza tangu alipoanza kuinoa Simba katika michuano yote zikiwemo mechi za kimataifa na zile za kirafiki.

Kwa matokeo hayo, Azam wanapanda hadi nafasi ya nne wakiwa cna pointi 14, sawa na Simba lakini Azam wakiwa wamecheza mchezo mmoja zaidi.

Azam FC hii inaongozwa na kocha Kally Ongala akisaidiana na Aggrey Morris ambao ni wakongwe wa Azam tangu wakiwa wachezaji na inaonekana wameirudisha timu hiyo katika mbio za ubingwa.







Toa comment

The post Simba Yaonja Uchungu wa Mwiko, Yapigwa na Azam Uwanja wa Mkapa appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/58443/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT