Skip to main content

SIMBA INA KIBARUA KINGINE KIZITO KIMATAIFA

SIMBA imetinga hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao 4-1 dhidi ya de Agosto ya Angola ina kibarua kingine kusaka nafasi ya kutinga hatua ya robo fainali.

Chini ya Kocha Mkuu, Juma Mgunda ambaye ni mzawa mechi nne kashinda zote akishuhudia kipa namba moja Aishi Manula akitunguliwa bao moja.

Ni Moses Phiri yeye amemshuhudia akifunga jumla ya mabao matano kwenye mechi hizo nne akiwa ni namba moja kwa watupiaji ndani ya kikosi cha Simba.

Droo ya upangaji wa timu ambazo zitakutana na Simba kimataifa kwenye hatua ya makundi inatarajiwa kufanyika Novemba mwaka huu nchini Misri.

Mechi za hatua za awali zinatarajiwa kuanza kuchezwa Februari 10 hadi Aprili Mosi 2023.

Ni timu 16 zimeshapatikana kwenye hatua hiyo ya makundi ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Soka la Afrika.

Miongoni mwa timu ambazo inaweza kukutana nazo ni pamoja na Al Ahly,(Misri), Wydad Casablanca, (Morocco), Esperance, (Tunissia) au Raja Casablanca, (morocco) ambazo zipo poti namba moja.

Poti namba mbili ni Mamelod Sundowns, (Afrika Kusini), Zamalek, (Misri), Horoya, (Guinea), na Petro Atletico Luanda, (Angola).

Poti namba 4 ni Cotton Sport, (Cameroon), Al Merreikh, (Sudan), Vipers, (Uganda) na mshindi kati ya AS Vita na RC Kadiogo, (Burkina Faso).

The post SIMBA INA KIBARUA KINGINE KIZITO KIMATAIFA appeared first on Saleh Jembe.

The post SIMBA INA KIBARUA KINGINE KIZITO KIMATAIFA appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/y12sEjR

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT