Skip to main content

SERENGETI GIRLS WAMETIMIZA MALENGO KOMBE LA DUNIA

BAKARI Shime, Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Wasichana chini ya miaka 17, Serengeti Girls amesema baada ya kufuzu robo fainali ya Kombe la Dunia Wanawake U 17, wametimiza malengo.

Serengeti Girls imefuzu hatua hiyo baada ya kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Canada na mtupiaji wa Tanzania ni Veronica Mapunda dakika ya 35.

Ni mara ya kwanza kwa Serengeti Girls kushiriki michuano hiyo inayofanyika India na imemaliza nafasi ya pili kwenye kundi D.

Shime amesema:”Kwenye mchezo wetu ambao ulitupa nafasi ya kufuzu robo fainali ilikuwa ni kazi kubwa kwa wachezaji kwa kuwa tulikuwa nyuma kwa bao moja lakini tulipambana kupata bao.

“Pongezi kwa wachezaji wangu kwa kujituma na kuonesha juhudi kubwa uwanjani mpaka kufanikiwa kufuzu robo fainali na ushindi huu ni kwa ajili ya Watanzania na tumefanikiwa kufikia malengo yetu,” amesema.

Mchezo ujao wa Serengeti ni dhidi ya Colombia ambao unatarajiwa kuchezwa kesho Oktoba 22 ambao utakuwa ni wa hatua ya robo fainali.

The post SERENGETI GIRLS WAMETIMIZA MALENGO KOMBE LA DUNIA appeared first on Saleh Jembe.

The post SERENGETI GIRLS WAMETIMIZA MALENGO KOMBE LA DUNIA appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/58037/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT