Skip to main content

Nabi Atoa Masharti Yanga Kuwaua Club Africain Uwanja wa Mkapa Kombe la Shirikisho




Nabi Atoa Masharti Yanga Kuwaua Club Africain Uwanja wa Mkapa Kombe la Shirikisho

Kocha Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi akiongea jambo  na msadizi wake Cedrick Kaze.

WAKATI viongozi na mashabiki wa Yanga wakiumiza vichwa kuona namna ya kutinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika, kocha mkuu wa timu hiyo, Nasreddine Nabi ameutaka uongozi kuhakikisha wanamtuma mtu mapema kwenda nchini Tunisia ili kuweka mambo sawa ikiwemo kumletea mbinu za kuwaua Club Africain.

Novemba 2, mwaka huu, Yanga itakutana na Club Africain ya Tunisia kwenye mchezo wa mtoano wa Kombe la Shirikisho Afrika, utakaopigwa Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, kisha marudiano ni Novemba 9 nchini Tunisia. Mshindi wa jumla atafuzu makundi ya michuano hiyo.

Chanzo chetu kutoka Yanga, kimeliambia Spoti Xtra kuwa: “Nabi amedhamiria kushinda mchezo wetu dhidi ya Club Africain, maana tayari ameutaka uongozi kuhakikisha wanamtafuta mtu anayeweza kwenda Tunisia mapema kuwashuhudia wapinzani wetu ili kuleta mbinu ambazo zitasaidia kuwamaliza.

“Tayari maagizo yake yamefanyiwa kazi na kwamba wamemtaka kukaa naye chini baada ya mchezo dhidi ya KMC, kisha wapange kama ni kocha wa viungo au msaidizi atakayeenda huko Tunisia kuifanya kazi hiyo,” kilisema chanzo hicho.

Kwa upande wa Nabi, amesema: “Tunaelewa kuwa ratiba yetu imebana, tunafanya kila jitihada ili kuendana na hali halisi tunayokabiliana nayo kwa sasa. “Lengo kubwa ni kuhakikisha tunashinda pamoja na kwamba tuna mechi ngumu mbele yetu, huo ndio ukweli tunaopaswa kukabiliana nao ili tufanikiwe.

Stori na MUSA Mateja







Toa comment

The post Nabi Atoa Masharti Yanga Kuwaua Club Africain Uwanja wa Mkapa Kombe la Shirikisho appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/0tyXhQ8

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT