Skip to main content

Mayele: Hatujakata Tamaa Mashindano ya Kimataifa Tutakiwasha Kombe la Shirikisho Afrika




Mayele: Hatujakata Tamaa Mashindano ya Kimataifa Tutakiwasha Kombe la Shirikisho Afrika

Mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele.

FISTON Mayele, mshambuliaji wa Yanga, amesema kushindwa kufuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika, sio mwisho wa kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.

Juzi Jumapili, Yanga ilitolewa na Al Hilal kwa jumla ya mabao 2-1, sasa imeangukia Kombe la Shirikisho Afrika.

Akizungumza na Spoti Xtra, muda mfupi baada ya msafara wa Yanga kurejea Dar ukitokea Sudan, nyota huyo amesema bado wana nafasi ya kufanya vizuri kimataifa.

“Tumeshindwa kufikia malengo ya kufika hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika, hatujapenda ila tuna nafasi katika Kombe la Shirikisho Afrika, huko tutapambana kufanya vizuri.

“Tulijadili na wachezaji baada ya mchezo tukakubaliana kwamba bado tuna kazi ya kufanya Kwa ajili ya mashabiki na kutimiza malengo kwani mashabiki wanahitaji ushindi Jambo ambalo nasi tunalihitaji pia. Hatujakata tamaa,” alisema Mayele.

Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said alisema: “Makosa tutafanyia kazi ili kuwa bora na tunaamini kuwa tutafanya vizuri kwenye Kombe la Shirikisho Afrika ambako nako ni mashindano ya kimataifa.”

Kiungo wa Yanga, Bernard Morrison, alisema: “Tulijipanga kwa ajili ya kushinda, lakini haikuwa hivyo, tumepoteza lakini bado tupo kwenye mashindano ya kimataifa, hatujatolewa moja kwa moja.”

STORI; LUNYAMADZO MLYUKA







Toa comment

The post Mayele: Hatujakata Tamaa Mashindano ya Kimataifa Tutakiwasha Kombe la Shirikisho Afrika appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/57945/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT