Skip to main content

MANCHESTER UNITED, CHELSEA ZAMUWANIA LEAO

NI Manchester United pamoja na Chelsea zimeingia katika mpango wa kuwania saini ya winga wa AC Milan na timu ya Taifa ya Ureno Rafael Leao.

Leao alikuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Italia Serie A msimu uliopita, amebakisha miezi 18 katika mkataba wake alionao kwa sasa na mabingwa watetezi wa Ligi hiyo AC Milan.

Taarifa kutoka katika viunga vya Milan zinabainisha kuwa Leao amegoma kuongeza mkataba mpya wa miaka mitano aliopewa na uongozi wa AC Milan akiwa kwenye mpango wa kusepa.

Kwa muda mrefu Klabu ya Chelsea imekuwa ikihusishwa na dili la kumsajili Leao ambapo taarifa zinadai kuwa Chelsea iliulizia huduma ya winga huyo katika majira ya kiangazi ya usajili lakini AC Milan ikatia ngumu kuwa mchezaji huyo hauzwi.

Chelsea pamoja na Man United zote zinatarajiwa kurejea na ofa mpya majira ya dirisha kubwa la uhamisho la kiangazi ili kuweza kupata saini ya winga huyo mwenye kasi na ubunifu mkubwa.

The post MANCHESTER UNITED, CHELSEA ZAMUWANIA LEAO appeared first on Saleh Jembe.

The post MANCHESTER UNITED, CHELSEA ZAMUWANIA LEAO appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/SxCRp9I

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT