Skip to main content

Makatibu CCM mtegoni

Na Norah Damian, Mtanzania Digital

Ni mtego! ndivyo unavyoweza kusema baada ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo kusema watachukua hatua dhidi ya watendaji wanaoshindwa kusimamia mali za chama.

Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo, akikata utepe wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba ya katibu wa chama hicho Mkoa wa Dar es Salaam inayojengwa Kigamboni.

Mwaka 2017 chama hicho kiliunda tume iliyokuwa na jukumu la kufuatilia mali za chama kote nchini na baada ya kukabidhiwa ripoti pamoja na mambo mengine kilielekeza zitafutwe nyaraka za kisheria za umiliki wa baadhi ya maeneo.

Akizungumza Oktoba 22,2022 baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba ya katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam na jengo la CCM Wilaya ya Kigamboni, Chongolo, amesema kasi ya kutafuta nyaraka za kisheria za umiliki wa maeneo ya chama imepungua.

“Inasikitisha kuona mali ambazo tumezimiliki kwa miaka mingi mtu anajitokeza na kusema hapa kwangu, wenye mali ambao ni chama ngazi husika wanatakiwa kusimamia wapo, wamekaa kimya na baadhi wameacha na kuona si sehemu ya wajibu wao…tutakapoanza kuchukua hatua zitaelekezwa kwa mtendaji wa eneo husika,” amesema Chongolo.

Katika hatua nyingine Chongolo amekemea tabia ya baadhi ya watu wanaoendeleza rushwa katika uchaguzi na kusababisha wenye dhamira ya kweli ya uongozi kukosa nafasi.

“Chama hiki kina watu wazuri wa kuwa viongozi, tatizo ni baadhi yetu kutengeneza miundombinu haramu ya kuwadhibiti watu wazuri kupata uongozi.

“Tutapitia kila jina, tutapitia maelezo binafsi ya kila mgombea na tutajiridhisha ili tupate viongozi wenye dhamira ya kweli ya kuendeleza utumishi wa chama chetu mbele.

“Vikao vitakavyoenda kuketi Dodoma vitatenda haki, vitafanya kazi bila upendeleo, wale mtakaobakia msitengeneze nongwa, chama kina nafasi nyingi msipate shida…usipotosha leo utatosha kesho,” amesema Chongolo.

Kuhusu ujenzi huo Chongolo amewapongeza viongozi na wanachama kwa kujitoa na kuwataka wajitahidi kukamilisha haraka.

Ujenzi wa nyumba ya katibu wa mkoa ulianza Juni mwaka huu na mpaka sasa Sh milioni 90 zimetumika na wanatarajia itakamilika Desemba mwaka huu.

Kwa upande jengo la CCM Kigamboni, Katibu wa CCM Wilaya ya Kigamboni, Stanley Mkandawile, amesema ujenzi ulianza mwaka 2020 na mpaka sasa fedha zilizotumika ni Sh milioni 190.7 na kwamba zinahitajika Sh milioni 95.3 kuukamilisha.

Katika hafla hiyo Mbunge wa Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile, amemuomba Chongolo kuweka msukumo kwenye Mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam (DMDP) ili waweze kupata barabara kabla ya 2025.

“Tunaomba pia tuangalie upya tozo za daraja, watu wanasema Kigamboni unaingia kwa fedha unatoka kwa fedha,” amesema Dk. Ndungulile.

The post Makatibu CCM mtegoni appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/58176/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT