Skip to main content

Kocha wa Yanga: Mashabiki Tulieni, Kazi Haijaisha, Tunaenda nKuwashangaza Al Hilal Kwao



Kocha wa Yanga: Mashabiki Tulieni, Kazi Haijaisha, Tunaenda nKuwashangaza Al Hilal Kwao

Kocha mkuu wa Yanga, Nasredine Nabi

NASREDDINE Nabi, Kocha Mkuu wa Yanga, ana kibarua cha kwenda ugenini kusaka ushindi dhidi ya Al Hilal baada ya mchezo wa kwanza kutoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1, lakini amewaambia Wanayanga watulie, kwani kazi haijaisha.

Jana Jumamosi kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar, kulikuwa na mchezo wa nguvu nyingi na akili kati ya wenyeji Yanga dhidi ya Al Hilal ya Sudan wa Ligi ya Mabingwa Afrika, ambapo dakika 45 za mwanzo zilikamilika kwa timu hizo kushindwa kufungana, huku kipindi cha pili ndipo mabao yakipatikana.

Fiston Mayele alianza kuifungia Yanga bao dakika ya 50 akiwa nje ya 18 akitumia pasi ya Khalid Aucho.

Bao hilo lilidumu hadi dakika ya 67 baada ya Al Hilal inayonolewa na Kocha Mkuu, Florent Ibenge kusawazisha kupitia Mohamed Youseif.

Mashabiki wa Yanga wakifanya yao Uwanja wa Mkapa.

Yanga ina kibarua kingine cha kwenda kusaka ushindi ugenini ili kutinga hatua ya makundi kwenye mchezo wa marudio unaotarajiwa kuchezwa nchini Sudan Oktoba 16.

Kuelekea mchezo wa marudiano, Kocha Nabi amewaambia Wanayanga watulie kwani wanaenda Sudan kuwashangaza wenyeji wao na kufuzu hatua ya makundi.

Katika mchezo wa jana, kiungo wa Yanga, Stephane Aziz Ki ambaye alianza kikosi cha kwanza, alipata nafasi tatu ambazo mashuti yalilenga lango dakika ya 8, 38 na 41.

Mayele shuti lake moja ambalo lililenga lango, ndilo lilikuwa bao, huku mengine matatu yakishindwa kulenga lango.

Wakati Yanga ikilazimishwa sare ya 1-1, Kipanga nayo ilishindwa kufungana na Club Africain, ukiwa ni mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika hatua ya kwanza uliochezwa Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Timu hizo zitarudiana wikiendi ijayo nchini Tunisia.

STOLI NA ISSA LIPONDA NA KAZIJA THABIT







Toa comment

The post Kocha wa Yanga: Mashabiki Tulieni, Kazi Haijaisha, Tunaenda nKuwashangaza Al Hilal Kwao appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/57060/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT