Skip to main content

Kisa Yanga, Klabu ya Simba Kukumbwa na Adhabu Kutoka TFF




Kisa Yanga, Klabu ya Simba Kukumbwa na Adhabu Kutoka TFF

Kiungo Mkabaji wa Simba SC Jonas Mkude akipambana na Kiungo mshambuliaji wa Klabu ya Yanga Stephen Aziz Ki

KLABU ya Simba SC inasubiri adhabu kutoka katika Bodi ya Ligi kwa sababu ya kufikisha kadi za njano tano (5) katika mchezo mmoja ambazo ni kinyume na kanuni.

Katika mchezo wa jana Jumapili, Oktoba 23, 2022, Derby ya Kariakoo, klabu ya Simba SC imepata kadi za njano tano huku watani wao wa jadi, klabu ya Yanga SC ikipata kadi za Njano nne (4).

Mwamuzi wa mchezo, Ramadhani Kayoko ametoa kadi za njano 9 kama ifuatavyo;

Okra Augustine (Simba)

Feisal Salum (Yanga)

Mzamiru Yassin (Simba)

Mohamed Hussein (Simba)

Khalid Aucho (Yanga)

Aziz Ki (Yanga)

Jonas Mkude (Simba)

Djuma Shabani (Yanga)

Habib Kyombo (Simba).

Klabu ya Simba kukumbwa na adhabu kutoka TFF

Kwa mujibu wa kanuni ya Ligi, klabu ikipata kadi za Njano tano au zaidi katika mchezo mmoja, klabu hiyo hutafsiriwa kuwa na utovu wa nidhamu.

Fahamu kwamba, kwa mujibu wa kanuni za Ligi Kuu Tanzania Bara, ni Bodi ya Ligi pekee ndio yenye mamlaka ya kutoa adhabu hiyo na si vinginevyo.

Mpaka kipenga cha mwisho, timu zote zimetoshana nguvu kwa kutoka sare ya kufungana bao 1-1. Simba ndio walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Augustine Okrah dakika 15 kabla ya Aziz Ki kuisawazishia Yanga kwa mkwaju wa adhabu dakika ya 45 ya mchezo.







Toa comment

The post Kisa Yanga, Klabu ya Simba Kukumbwa na Adhabu Kutoka TFF appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/58267/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT