Skip to main content

Injinia Hersi: Wachezaji Wametuapia Kuifunga Simba Kesho Kutwa Jumapili



Injinia Hersi: Wachezaji Wametuapia Kuifunga Simba Kesho Kutwa Jumapili

Rais wa Klabu ya Yanga, Eng Hersi Said.

WACHEZAJI wa Yanga kwa pamoja wamewaahidi viongozi wa timu hiyo, kupambana kwa dakika 90 ili kuhakikisha wanarejesha furaha ya mashabiki, watakapovaana na Simba keshokutwa Jumapili.

Dabi hiyo inatarajiwa kuzikutanisha Yanga na Simba katika mchezo wa raundi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.

Timu hiyo, juzi Jumatatu ilirejea kambini Kijiji cha Avic Town, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam mara baada ya kutoka kutolewa na Al Hilal katika mchezo wa raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Akizungumzana Championi Ijumaa, Hersi alisema kuwa mara baada ya timu hiyo kuingia kambini uongozi ulifanya kikao na wachezaji ambao walionekana kusikitishwa na kuumizwa na matokeo dhidi ya Al Hilal ambayo yamewakera mashabiki wa Yanga.

Hersi alisema kuwa katika kuelekea dabi hiyo, wachezaji wameahidi kupambana kufa au kupona ili kuhakikisha wanapata matokeo mazuri yatakayorudisha imani ya Wanayanga.

Aliongeza kuwa mara baada ya kikao hicho, wachezaji hao walihimizana kila mmoja kutimiza majukumu yake ya uwanjani pale atakapopata nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza.

“Wachezaji wanajutia makosa yao waliyoyafanya ambayo yamesababisha kushindwa kufikia malengo ya kufuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu.

“Hivyo wameahidi kurejesha imani ya mashabiki wa Yanga kwa kushinda katika dabi hii, ni baada ya kuondolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika, kila mmoja ameahidi kuipambania timu katika mchezo huo.

“Tunafahamu haitakuwa rahisi, lakini wachezaji wenyewe upande wao wametoa ahadi hiyo kubwa ambayo ikifanikiwa, basi ninaamini mashabiki watarudisha Imani kwa timu yao,” alisema Hersi.

STORI: WILBERT MOLANDI NA MUSA MATEJA







Toa comment

The post Injinia Hersi: Wachezaji Wametuapia Kuifunga Simba Kesho Kutwa Jumapili appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/dmahr2B

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT