Skip to main content

GF Truck yapongezwa kwa kusaidia uchangiaji damu salama Geita

Na Anna Ruhasha Geita

Kampuni inayouza magari makubwa ya mizigo pamoja na mitambo mbalimbali ya ujenzi ya GF Trucks & Equipment imewezesha upatikanaji wa chupa za damu salama 25 kwa ajili kuunga mkono uchangiaji wa damu nchini ili kuokoa uhai wa wagonjwa wenye uhitaji wa mkoani Geita.

Wananchi wakiendelea na uchangiaji damu salama mkoani Geita.

Hayo yameelezwa na Meneja Masoko na Mahusiano Kampuni ya GF Trucks, Smart Deus wakati Waziri wa Madini, Dk. Doto Biteko kutembelea banda hilo katika maonesho ya tano ya kitaifa ya teknolojia ya madini yanayoendelea mkoani Geita.

“Mhe. Waziri GF Trucks tunaadhimisha miaka 15 tangu tumeanza kutoa huduma kwa jamii na katika maonesho haya tumedhamini upatikanaji wa damu salama chupa 25, lakini pia kwa wateja watakaonunua bidhaa kwetu katika maonesho tutawafanyia huduma(service) bure mteja yeye ataweza kununua vipuri,“ amesema Deus.

Aidha, Muuguzi Kitengo cha damu salama katika Hospitali ya Mkoa wa Geita, Angelina Swai ameishukuru GF Truck kwa kudhamini chakula na vinywaji kwa vikundi vya wasanii na Bodaboda waliojitokeza kuchangia jumla ya chupa 25 za damu ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa damu salama mkoani humo.

“Mh Waziri nikukalibishe katika banda letu la kuchangia damu salama lakini pia nitumie nafasi hii kuishukuru kampuni ya GF Trucks ambayo imewezesha kwa kiwango kikubwa upatikanaji wa chupa hizi za damu, hata hivyo tangu maonesho ya teknolojia ya madini yameanza hapa mkoani kwetu zaidi ya chupa za damu salama 148 zimepatika,” amesema Swai.

Waziri wa Madini, Dk. Doto Biteko akizungumza katika na waandishi wa Habri alipotembelea banda la kampuni ya GF Truck.

Waziri wa Madini Dk. Doto Biteko ameipongeza kampuni ya GF Truck kwa uzalendo wake katika jamii kwa kutumia maonesho hayo kuwezesha upatikanaji wa damu salama, huku akiziomba kampuni zilizopo katika maonesho hayo kuiga kwa GF Trucks kusaidi uchangiaji wa damu salama ili kuokoa maisha ya watu.

“Ni wapongeze sana GF Truck na msichoke kuisaidia jamii kwa mambo mbalimbali hususan jamii ya wachimbaji wadogo wadogo wa madini ili sekta hii iweze kukua na kuchangia pato la taifa,“ amesema amesema Waziri Biteko.

Kampuni hiyo ya GF Truck mbali na kuwezesha uchangiaji damu salama katika maonesho hayo, wao pia ni moja ya wafadhili wakubwa wa maonesho ya 5 ya kitaifa ya teknolojia ya madini na uwekezaji yanayoendelea mkoani Geita.

The post GF Truck yapongezwa kwa kusaidia uchangiaji damu salama Geita appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/56425/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT