Skip to main content

FEI TOTO, MORRISON NA AZIZ KI WAPEWA KAZI KIMATAIFA

VIUNGO wa Yanga ikiwa ni pamoja na Aziz KI, Feisal Salum, Bernard Morrison, Khalid Aucho wamepewa kazi maalumu kuelekea kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Hilal.

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa nchini Sudan, Jumapili, Oktoba 16,2022 saa 2:00 usiku baada ya ule uliochezwa Uwanja wa Mkapa,ubao usoma Yanga 1-1 Al Hilal.

Nasreddine Nabi, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa kila mchezaji ana jukumu la kutimiza kazi yake uwanjani ili kuipa timu matokeo.

Kazi kubwa kwa viungo hao ni kutengeneza nafasi nyingi kuelekea lango la wapinzani ili washambuliaji wa timu hiyo wafanikiwe kufunga.

Ikumbukwe kwamba Nabi amekuwa akipenda kumtumia mshambuliaji Fiston Mayele mwenye mabao 7 kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye hatua ambayo Yanga ipo.

Nafasi yake imekuwa ikichukuliwa na Heritier Makambo ambaye amekuwa na nafasi finyu kikosi cha kwanza msimu huu wa 2022/23.

Kazi nyingine ambayo wamepewa viungo hao ni kuhakikisha wanatumia mapigo huru kwa umakini ikiwa ni pamoja na kona pamoja na faulo ambapo jukumu la kupiga kona limekuwa likimuangukia kiungo Aziz KI.

“Tuna mchezo mgumu mbele yetu ambao ni dhidi ya Al Hilal, kwenye mpira wa miguu kila kitu kinawezekana na ambacho kinatakiwa kwa sasa ni kila mchezaji kutimiza majukumu yake.

“Ninajua kuhusu uwezo wa viungo ambao wapo pamoja na washambuliaji, muhimu kwenye nafasi tutakazopata kuzitumia kwani kwenye hatua za Ligi ya Mabingwa huwa zinapatikana nafasi chache ambazo ni muhimu kuzitumia,”.

The post FEI TOTO, MORRISON NA AZIZ KI WAPEWA KAZI KIMATAIFA appeared first on Saleh Jembe.

The post FEI TOTO, MORRISON NA AZIZ KI WAPEWA KAZI KIMATAIFA appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/57426/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT