Skip to main content

EWURA yajipanga kuimarisha nishati ya mafuta vijijini

Na Yohana Paul, Geita

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) wamebainisha wameweka mazingira rafiki kuhakikisha huduma ya mafuta yanapatikana nchi nzima ili kuimarisha huduma ya usafiri kwa vyombo vya moto vijijini.

Meneja wa Ewura Kanda ya Ziwa, Mhandisi George Mhina amebainisha hayo wakati akizungumuza na waandishi wa habari katika viwanja vya Bombambili mjini Geita yanapofanyika Maonyesho ya Tano ya Teknolojia ya madini.

Mhandisi Mhina amesema “Sisi Ewura kwa sasa tunahimiza sana ujenzi wa vitruo vya mafuta vijijini, ili kuepuka wananchi kutumia mafuta kwenye vidumu, na tumetengeneza kanuni mahususi kwa hiyo tumerahisisha vigezo na mashariti.

“Ndio maana ukiona vituo vya mjini huku gharama yakekujenga inaweza kuwa Sh milioni 300 mpaka 500, sasa kwa mtanzania wa kawaida kule kijijini ambako kuna bodaboda na shughuli zingine vigezo tumevirahisisha zaidi.

“Mtu akiwa na Sh milioni 40 mpaka 50, unaweza ukajenga kituo cha mafuta katika ngazi ya kijiji na wananchi wakapata mafuta bora na kwa gharama ambayo tunaipanga (bei elekezi).”

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Ally Gugu akizungumuza baada ya kukagua mabanda ya maonyesho hayo amesema Ewura ni miongoni mwa taasisi muhimu hivo waendelee kutekeleza wajibu wao.

“Wenzetu wa Ewura kazi yao kubwa ni kuhakikisha tunakuwa na nishati yenye viwango,ili tunapowavutia wawekezaji basi waweze kuja kuwekeza nchini na wapate huduma hizo zenye viwango ambazo wao wanazisimamia,” amesema Gugu.

Amesema Wizara inaunga mkono juhudi za Ewura kuhakikisha huduma ya mafuta inapatikana kila kona ya nchi hivo wameweka sera wezeshi kwa wawekezaji kujenga vituo vya mafuta vya chini, kati na vikubwa maeneo ya vijijini.

The post EWURA yajipanga kuimarisha nishati ya mafuta vijijini appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/Fk12vOM

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT