Skip to main content

Azam FC yavunja rekodi ya ‘Mzizima Derby’ iliyodumu kwa miaka 5

MZIZIMA ‘Derby’ imetamatika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kwa wenyeji Azam FC kushinda bao 1-0 lililofungwa dakika ya 35 ya kipindi cha kwanza na mshambuliaji, Prince Dube. Ushindi huu ni wa kwanza kwa Azam dhidi ya Simba baada ya kupita miaka mitano tangu mara ya mwisho iliposhinda pia bao 1-0, Januari 28, 2017, lililofungwa na John Bocco ambaye kwa sasa ni nahodha kwenye kikosi cha Simba. Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote mbili kushambuliana kwa zamu huku wenyeji Azam wakiendelea kutumia njia Ile Ile ya kushambulia kwa kushtukiza. Dakika ya 60, Azam ilifanya mabadiliko ya kuwatoa Kipre Junior na Kenneth Muguna huku nafasi zao zikichukulia na Idd Suleiman ‘Nado’ na Yahya Zayd ili kuongeza nguvu katika ushambuliaji. Kwa upande wa Simba chini ya Kocha Mkuu, Mgunda alifanya mabadiliko pia dakika ya 65 kwa kumtoa Habib Kyombo ambaye tangu mwanzo hakuwa na mchezo mzuri na nafasi yake ikachukuliwa na nahodha, John Bocco. Simba iliendelea kufanya mabadiliko ambapo iliwatoa Augustine Okrah, Jonas Mkude huku nafasi zao zikichukuliwa na Peter Banda na Kibu Denis kwa lengo la kuongeza nguvu eneo la ushambuliaji. Kwa upande Azam nao waliendelea kufanya mabadiliko ambapo ilimtoa mfungaji wa bao Prince Dube huku nafasi yake ikichukuliwa na Rodgers Kola wakati Nathaniel Chilambo akiingia pia kuchukua nafasi Ayoub Lyanga. Simba ilifanya tena mabadiliko ya kumtoa kiungo wake Nassoro Kapama huku nafasi yake ikichukuliwa na winga mshambuliaji, Pape Sakho. Licha ya mabadiliko hayo ya kiufundi kwa timu zote ila ni Azam chini ya Kaimu Kocha wake Mkuu, Kali Ongala aliyepewa nafasi hiyo baada ya kuondoka Mfaransa, Denis Lavagne ndiye ambaye amenufaika zaidi na ushindi huu. Kwa matokeo haya yanaifanya Simba kupoteza mchezo wake wa kwanza msimu huu chini ya Juma Mgunda baada ya kuanza vizuri tangu alipochukua mikoba ya Mrsebia, Zoran Maki. Kikosi cha Azam kilichoanza ni Ali Ahamada, Lusajo Mwaikenda, Bruce Kangwa, Daniel Amoah, Edward Manyama, Isah Ndala, Ayoub Lyanga, James Akaminko, Prince Dube, Kenneth Muguna na Kipre Junior. Wachezaji wa akiba ni Wilbol Maseke, Nathaniel Chilambo, Cleophance Mkandala, Yahya Zayd, Tape Edinho, Idd Nado, Rodgers Kola, Abdallah Kheri na Idris Mbombo. Kikosi kamili cha Simba kilichoanza ni Aishi Manula, Erasto Nyoni, Mohamed Hussein ‘Tshabala’, Joash Onyango, Henock Inonga, Jonas Mkude, Clatous Chama, Nassoro Kapama, Habib Kyombo, Moses Phiri na Augustine Okrah. Wachezaji wa akiba ni, Beno Kakolanya, Gadiel Michael, Kennedy Juma, Mohamed Quattara, Victor Akpan, Peter Banda, John Bocco, Kibu Denis na Pape Sakho.

The post Azam FC yavunja rekodi ya ‘Mzizima Derby’ iliyodumu kwa miaka 5 appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/58435/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT