Skip to main content

WFP inapanga kutoa msaada wa chakula kwa  watu 700,000 nchini Zimbabwe

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) linapanga kutoa msaada wa chakula unaowalenga watu 700,000 nchini Zimbabwe kuanzia Oktoba huku athari za mavuno duni na vita vya Ukraine vikiendelea kuonekana, afisa mmoja amesema.

Serikali ya Zimbabwe inafanya kazi na mashirika ya msaada ili kutoa chakula kwa watu milioni 3.8, WFP ilisema.

Nchi hiyo ya kusini mwa Afrika imekuwa ikijitahidi kujilisha tangu mwaka 2000, wakati kiongozi wa zamani Robert Mugabe alipotetea unyakuzi wa mashamba yaliyokuwa yanamilikiwa na wazungu ili kuwapa makazi watu weusi wasio na ardhi.

Serikali ya Zimbabwe imesema inatarajia mavuno ya zao lake kuu la mahindi kupungua kwa karibu nusu mwaka huu, hadi tani milioni 1.56 kutoka rekodi ya msimu uliopita ya tani milioni 2.72, kutokana na mvua duni katika msimu wa kilimo wa 2021-22.

Nchi inahitaji tani milioni 2.2 za mahindi kila mwaka kwa matumizi ya binadamu na mifugo.

The post WFP inapanga kutoa msaada wa chakula kwa  watu 700,000 nchini Zimbabwe appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/urNHIDK

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT