Skip to main content

Watoto 287,512 kupatiwa chanjo ya Polio Songwe

Na Denice Sikonde, Songwe

Serikali mkoani Songwe imepanga ktoa chanjo ya polio kwa watoto 287,512 wenye umri chini ya miaka mitano katika kampeni itakayofanyika kwa siku Nne kuanzia Septemba Mosi hadi 4, mwaka huu.

Hayo amesema Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Cosmas Nshenye ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mbozi katika kikao cha afya ya msingi ngazi ya mkoa kilichofanyika Agosti 30, na kujadili mikakati ya utekelezaji wa kampeni ya polio.

Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho.

Nshenye amesema kampeni hiyo ya polio watalamu watapita nyumba kwa nyumba na maeneo yote yenye watoto wenye umri chini ya miaka mitano pamoja na vituo vya kutolea huduma za afya ili kufikia malengo ya kuwakinga watoto wote dhidi ya ugonjwa hatari wa polio.

Nshenye ametoa wito kwa wazazi/walezi wenye watoto wa umri chini ya miaka 5 kuhakikisha mtoto anapata chanjo ya matone ya Polio kwani Mtoto asiyepata chanjo Ni hatari kwa maisha yake na kwa jamii inayomzunguka.

Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani, Dk. Robert Hongo amesema kwa sasa Tanzania haina ugonjwa huo ila inachukua hatua usiingie nchini tangu utangazwe Januari 2022 nchini Malawi na Msumbuji ambazo ziko jirani na Tanzania na ukizingatia mwingiliano wa watu ni mkubwa hivyo hatua stahiki za kuwakinga watoto kwa chanjo ya matone ya polio ni muhimu.

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Happiness Seneda amesema ni vyema jamii ikajua athari za ungonjwa polio kwa upana wake ili waweze kujitokeza kwa wingi kuwapatia chanjo watoto wao.

“Baada ya Nchi kutoa chanjo ugonjwa huu ulipotea sasa watu wengi wanausikia tu, ni vyema jamii ikapata athari za ugonjwaa huu kwa undani,” amesema Seneda.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Dk. Boniface Kasululu amesema katika Kampeni hii ya chanjo ya polio inayoanza Septemba Mosi mwaka huu watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano watapata chanjo hata kama ametoka kupata chanjo hiyo siku moja kabla.

Pia, Dk. Kasululu amesema ata kama Mtoto alipata chanjo ya matone kwa ratiba yake ya kliniki lakini ndani ya siku nne za kampeni hii Mtoto huyo atapata chanjo tena.

Mratibu wa Chanjo Mkoa wa Songwe, Moses Lyimo amesema wamejipanga vizuri kuhakikisha kampeni inafanyika vizuri na kuwafikia watoto lengwa wote pamoja na kutoa elimu kwa wazazi/walezi kupitia vyombo vya Habari juu ya athari ya ugonjwa wa Polio kwenye jamii.

Kampeni hii ya polio ni ya nne tangu kutangazwa kwa ugonjwa huu nchini Malawi lengo kuchukua hatua ya kujikinga dhidi ya ugonjwa huu hatari.

The post Watoto 287,512 kupatiwa chanjo ya Polio Songwe appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/YTq7vIl

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT