Skip to main content

Tanzia ya Malkia Elizabeth II wa Uingereza

Alikuwa ni kiongozi wa muda mrefu katika utawala wa kifalme duniani na mwaka huu alisherehekea miaka 70 ya kushikilia taji hilo.

Mwandishi Henry Ridgwell anaangalia maisha ya mmoja wa viongozi walioheshimiwa sana duniani.

Alikuwa kiongozi pekee wa kifalme ambao waingerea wanaishi leo wamewahi kuwafahamu, ni mfano taifa, himaya yake na jumuiya ya madola. Alionyesha nguvu ya Uingereza na tabia yake muda mrefu kabla hata ya kujua atakuwa malkia.

Malkia Elizabeth II alisema:“Natangaza mbele yenu nyote kuwa maisha yangu yote, yawe marefu au mafupi, nitajitolea kuwahudumia na kwa huduma kwa familia yangu kubwa ya kifalme ambayo sote ndiyo tuko humo.”

Akiwa na umri wa miaka 25, Elizabeth aliingia katika uongozi wa kifalme baada ya kifo cha baba yake George wa sita, takriban miaka mitano tu baada ya kuolewa na mzaliwa wa Ugiriki, Prince Phillip.

Alishuhudia mabadiliko makubwa na ya kina katika jamii na teknolojia wakati wa utawala wa zaidi ya miongo saba, wakati ambapo alionya kuhusu hatari za kutu kuachana na maadili ya zamani wakati wakikumbatia fursa za uvumbuzi mpya.

Aliandika tweet yake ya kwanza mwaka 2014. Kuna rekodi chache ambazo hakuzivunja: alikuwa ni kiongozi wa muda mrefu duniani katika himaya ya kifalme.

((Richard Fitzwilliams, Mwandishi na Mchambuzi wa Masuala ya Kifalme))
“Kama mkuu wa Jumuiya ya Madola, malkia ana uhusiano na matukio yaliyopita. Mara nyingine ilikuwa ni matukio magumu kwasababu dhana ya ufalme, wakiangalia unyanyasaji wa kikoloni na ufalme. Lakini malkia alikuwa na wasi wasi, nadhani kwasababu ya nia yake ya dhati kwa taasisi.”

Aliwakilisha urafiki wa Uingereza kwa wale ambao walikuwa na thamini sawa na za Uingereza kama vile uhuru, usawa, na demokrasia. Kwajeshima alikabiliana na wale waliokuwa na mtizamo tofauti.

Kuonekana naye ilikuwa na maana ya kupata fursa nzuri na heshima kubwa.

Malkia wa Uingereza Elizabeth


Malkia wa Uingereza Elizabeth

Malkia pia alikuwa akikosolewa katika nchi yake mwenyewe. Wa Marengo wa kushoto walimlenga kama mfano wa taasisi ambayo haiku sawa katika enzi hii ya sasa, uhuru mambo leo na demokrasia duniani na mzigo kwa mlipa kodi wa Uingereza.

Kifo cha Princess Diana ambaye alikuwa maarufu sana kilikuwa ni fursa nzuri kwa wakosoaji wake kumshutumu kwa kuwa kimya na kuchukua muda kuelezea chochote.

Princess Diana


Princess Diana

Malkia Elizabeth II alieleza kuwa: “Ninachowaeleza hivi sasa, kama Malkia wenu na kama bibi, nasema haya kutoka kwenye moyo wangu. Kwanza, natoa heshima kubwa kwa Diana. Alikuwa mtu wa kipekee na binadamu mwenye kipaji.”

Prince William na Kate


Prince William na Kate

Ndoa ya mjukuu wake Prince William kwa Kate Middleton ilionyesha hiba ya ujana kwa taasisi hii ya enzi na enzi.

Wakati + Prince Harry alipomuoa muigizaji wa kimarekani Meghan Markle, Elizabeth alikuwa kiongozi wa familia ambaye alionekana kwenda ambayo ilikwenda na wakati katika umaarufu, mabadiliko na ulimwengu.

Lakini kulikuwa na maumivu siku za usoni. Mtoto wake wa pili wa kiume Prince Andrew alikuwa akichunguzwa akihusisha na mashtaka yaliyomhusu mtuhumiwa wa ngono kwa watoto.

Prince Harry na Mkewe Meghan


Prince Harry na Mkewe Meghan

Harry na Meghan waliamua kujiondoa kwenye familia ya kifalme huku kukiwa na shutumba za ubaguzi.

Kifo cha mume wake Elizabeth, Prince Phillip mwaka 2021 kilimuacha na picha ya kudumu: malkia ambaye anaomboleza peke yake – wakati janga la corona lilipoingia katika taifa lake.

Mwezi Septemba alimteua waziri mkuu wa tano wa Uingereza chini ya himaya yake – ikiwa ni tukio lake la mwisho la umma.

FILE -Malkia Elizabeth (Frank Augstein/Pool via Reuters)


FILE -Malkia Elizabeth (Frank Augstein/Pool via Reuters)

Malkia Elizabeth atakumbukwa kuwa ni mkuu katika history ya moja ya mataifa makubwa sana duniani, ikiwa ni daraja kati ya mataifa ambayo yalikuwa chini ya ukoloni wa Uingereza na mustakbali wa baadaye kama wahusika wakuu katika dunia inayobadilika sana kutoka ile ambazo yeye alizaliwa na ilivyo sasa.

FILE - Malkia Elizabeth II alipotembelea Ujerumani.


FILE – Malkia Elizabeth II alipotembelea Ujerumani.

Alipoitembelea Ujerumani mwaka 2015, alizungumzia kuhusu mabadiliko makubwa aliyoshuhudia.

Malkia Elizabeth II alimwambia rais: “Katika maisha yetu Rais, tumeona mambomabaya sana na pia mazuri katika bara letu. Tumeshuhudia jinsi mambo kwa haraka yanavyoweza kubadilika kwa uzuri, lakini pia tunafahamu kwamba tufanye kazi kwa bidi ili kuendeleza mafanikio yaliyopatikana baada ya vita vya dunia.”

Familia ya Malkia wa Uingereza


Familia ya Malkia wa Uingereza

Utamaduni wa ufalme wa Uingereza – ambao Elizabeth aliushikilia – sasa uko katika mikono ya wale watakao mrithi.
Lakini Uingereza inarithi jambo moja tofauti sana katika misingi ya demografia, utamaduni na uchumi.

Katika ulimwengu, dunia hii, kazi yao ni kuonyesha sura ya ukubwa ambayo haina mikanganyiko.

The post Tanzia ya Malkia Elizabeth II wa Uingereza appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/xsGO57I

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT