Skip to main content

Rais wa Gabon aomba Afrika kuweka mikakati ya kulinda mazingira

Hayo yamesemwa na Rais wa Gabon Ali Bongo kwenye kongamano la tatu la hali ya hewa la Afrika kwenye mji mkuu wa taifa hilo wa Libreville. Kwa mujibu wa shirika la habari la AP, Bongo ameongeza kusema kwamba maafisa wa Afrika pamoja na wataalam wengine wanahitaji kupasa sauti zao wakati wa kongamano la 27 la Umoja wa Mataifa litakalofanyika Misri mwezi Novemba.

Kongamano la wiki moja la Gabon limewaleta pamoja zaidi ya maafisa 1,000 wa serikali pamoja na wadau wengine wa mabadiliko ya hali ya hewa. Kongamano hilo linafanyika wakati Afrika inakabiliana na majanga kadhaa ya mazingira kama vile ukame kwenye baadhi ya mataifa ya Afrika mashariki na pembe ya Afrika, dhoruba ya mchanga pamoja na joto kupita kiasi kwenye eneo la Sahel pamoja na mafuriko na vimbunga vingine katikati , kusini na magharibi mwa Afrika.

The post Rais wa Gabon aomba Afrika kuweka mikakati ya kulinda mazingira appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/52248/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT