Queen Darleen: Acha Wanione Mjinga Baada ya Kuachana na Ndoa
Msanii wa Bongo Fleva aliye chini ya Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB), Queen Darleen.
Queen Darleen; ni msanii wa Bongo Fleva aliye chini ya Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB) ya Diamond Platnumz ambaye ameibuka kusema kwamba acha watu wamuone mjinga baada ya kuachana na ndoa.
Darleen ambaye alifunga ndoa na mfanyabiashara Isihaka Mtoro kabla ya mambo kwenda mrama anasema kuwa, baada ya kuchukua hamsini zake, kwa anaishi maisha yenye furaha kuliko wakati alipokuwa ameolewa.
Darleen amesema hayo wakati akitoa maoni yake kuhusu habari ya kusikitisha ya mwanamke wa Nigeria aliyefariki dunia wakati akikimbizana kwa gari na mume wake aliyekuwa na mchepuko ndani ya gari linguine.
Mwanamke aliyefariki alikuwa mwanasheria ambaye imeelezwa kuwa alikuwa anapitia manyanyaso ndani ya ndoa na pia mumewe husika alikuwa hajatulia, anaendekeza umalaya na kutoheshimu misingi ya ndoa.
Inadaiwa pia kwa sasa aliyekuwa mume wa Queen Darleen yupo na mwanamke mwingine ukiacha yule mke mkubwa, Sabra ambaye ilisemekana walimaliza tofauti zao za awali.
Toa comment
The post Queen Darleen: Acha Wanione Mjinga Baada ya Kuachana na Ndoa appeared first on soka letu.
source https://mjombazecoder.website/56054/




Comments
Post a Comment