Skip to main content

MZEE WA KUCHETUA KARUDI, KUWAKOSA SIMBA

KIUNGO wa Yanga, Bernard Morrison amezidi kuwa imara hali yake na tayari ameanza mazoezi na wachezaji wenzake.

Nyota huyo alipata maumivu kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam FC uliochezwa Uwanja wa Mkapa ambao waligawana pointi mojamoja.

Ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Yanga 2-2 Azam FC na Morrison aliyeyusha dakika 90 lakini alikuwa amepata maumivu.

Licha ya kuanza mazoezi nyota huyo hatacheza mechi tatu zinazofuata kwenye ligi za Yanga baada ya kufungiwa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Bodi ya Ligi iliyo chini ya Shirikisho la Mpira Tanzania, (TFF).

Sababu ya nyota huyo mwenye bao moja ndani ya ligi ambalo aliwatungua Coastal Union Uwanja wa Sheikh Amri Abeid ni kile kilichoelezwa kuwa alimkanyanga kwa makusudi mchezaji wa Azam FC, Lusajo Mwaikenda.

Miongoni mwa mechi ambazo Morrison atazikosa msimu huu ni pamoja na ule dhidi ya Simba unaotarajiwa kuchezwa Oktoba 23, Uwanja wa Mkapa.

Pia atawakosa Namungo na Ruvu Shooting kwenye mtiririko wa adhabu hiyo na ametozwa faini ya milioni moja.

The post MZEE WA KUCHETUA KARUDI, KUWAKOSA SIMBA appeared first on Saleh Jembe.

The post MZEE WA KUCHETUA KARUDI, KUWAKOSA SIMBA appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/GMIegZV

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT