Skip to main content

Mwili wa Malkia Elizabeth wawasili Edinburgh, Scotland

Awali, gari lililobeba mwili wa hayati Elizabeth, likiwa na maafisa wa kifalme na walinda usalama, liliondoka kwenye Kasri la Balmoral, muda mfupi kabla ya Jumapili adhuhuri, ukiwa ni mwanzo wa safari ndefu na ya mwisho, ya Malikia Elizabeth, aliyeaga dunia Alhamisi wiki jana, baada ya kushikilia wadhifa wa ufalme wa Uingereza kwa miongo saba.

Msafara wake ulionekana, kwa polepole ukipitia mabonde na milima ya Scotland, na mandhari iliyothaminiwa na marehemu , eneo ambapo alitumia wiki zake za mwisho za amani.

Katika miaka ya nyuma, malkia alionekana mara kwa mara akitembelea vijiji hivi vya mbali, alipokuwa akiishi katika Kasri la Balmoral, makao ambayo aliyapenda.

Wakazi walikusanyika kando ya barabara ili kumtazama kwa mara ya mwisho na kusema kwaheri.

Wengine alitulia na kuonyesha ukimya ambao ulikuwa ni ishara ya mshtuko ambao raia wa Uingereza walipata – na heshima ambayo marehemu Malikia alipewa wakati wa uhai wake.

Baadhi ya watu walirusha maua, huku wengine wakipiga vigelegele wakati gari la kubebea maiti lilipopita.

Wengi katika umati wa watu walibubujikwa na machozi.

The post Mwili wa Malkia Elizabeth wawasili Edinburgh, Scotland appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/54031/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT