Skip to main content

Mjadala wa kitaifa Chad kuendelea kwa siku 10 zaidi

Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, mjadala huo wa kitaifa unaohusisha makundi mbali mbali kwa lengo la kurejesha utawala wa kiraia ulianza mwezi uliopita, ukipangwa kumalizika Septemba 20. Tarehe ya mwisho sasa imesogezwa hadi Septemba 30. Mazungumzo hayo yameahirishwa mara kadhaa hapo mbeleni baada ya makundi yenye silaha pamoja na makundi ya upinzani kususia, yakidai kwamba mazungumzo hayo ni kati ya serikali na washirika wake wa karibu.

Rais wa Chad Mahamat Idriss Deby Itno anaongoza baraza la kijeshi lenye wajumbe 15, baada ya kuchukua madaraka, kufuatia kifo cha baba yake wakati akiwa kwenye uwanja wa vita dhidi ya waasi Aprili 2021. Kiongozi huyo amebuni mjadala wa kitaifa kwa nia ya kuitisha uchaguzi huru na wa kidemokrasia katika kipindi cha miezi 18. Kikao hicho hicho kufikia sasa hakijapiga hatua kubwa kuelekea kwenye malengo yake.

The post Mjadala wa kitaifa Chad kuendelea kwa siku 10 zaidi appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/53418/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT