Skip to main content

MFARANSA WA AZAM FC ANASUKA KIKOSI KAZI KIMATAIFA

DENIS Jean, Kocha Mkuu wa Azam FC raia wa Ufaransa amesema kuwa kwa sasa mpango kazi uliopo ni kuandaa utimamu wa kikosi hicho kuelekea kwenye mechi za kimataifa pamoja na ligi.

Kocha huyo ambaye amesaini dili la mwaka mmoja kuchukua mikoba ya Abdi Hamid Moallin mchezo wake wa kwanza wa ligi alishuhudia timu hiyo ikishinda bao 1-0 dhidi ya Mbeya City, Uwanja wa Sokoine.

Mfaransa huyo amesema: “Tuna muda mrefu ambao tutakaa kutokana na kutokuwa na mechi jambo ambalo tunafanya kwa sasa ni kufanya maandalizi na kucheza mechi za kirafiki ambazo zitatufanya tuwe imara.

“Tunahitaji kuwa na kikosi imara kwenye mechi zetu za kitaifa na kimataifa nina amini kwenye uwezo wa wachezaji wetu na wanazidi kuonyesha juhudi kwenye kazi,”.

Mchezo ujao wa Azam FC ni dhidi ya Tanzania Prisons unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Sokoine, Septemba 30.

Septemba 23, Azam FC ilicheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya TP Mazembe na zilitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1.

Tayari kikosi kimerejea Dar kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo wao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Tanzania Prisons.

The post MFARANSA WA AZAM FC ANASUKA KIKOSI KAZI KIMATAIFA appeared first on Saleh Jembe.

The post MFARANSA WA AZAM FC ANASUKA KIKOSI KAZI KIMATAIFA appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/b8Z4Du3

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT