Skip to main content

Meridianbet Waunga Mkono Kampeni ya Buku ya Hedhi Salama

Meridianbet wameunga mkono jitihada za kampeni ya Buku ya Hedhi salama inayoratibiwa na Shufaa Hemed Nasoro.

Kampeni hii ilikuwa imelenga kuchangisha michango ya kiwango cha angalau shilingi elfu moja kuwasaidia mabinti ambao wanapata changamoto za kumudu gharama za taulo za kike.

Meridianbet, ambao ni wadau wakubwa wa shughuli za kijamii, wanaona umuhimu wa hedhi salama kwa mabinti, na katika kuhakikisha hilo linafanikiwa hawakusita kuwashika mkono waratibu wa kampeni hii.

Kampeni hii inawalenga mabinti na wanawake wanaoshindwa kumudu gharama za taulo za kike Tanzania nzima, waratibu wakiwa wanalenga kuyafikia maeneo mengi yenye uhitaji ikiwa ni pamoja na vijijini.

Wakati kampeni ikitoa fursa ya kila mtu kuchangia kwa kutoa mchango wa shilingi elfu moja kuiwezesha kampeni hii, Meridianbet wametoa boksi 16, na kila boksi ikiwa na pakiti 30 za taulo za kike.

Akizungumza kwa niaba ya Meridianbet, Meneja wa Masoko wa Meridianbet bwana Twaha Mohammed amesema wanafurahi kuwaongezea kujiamini.

“Sisi tumekuwa na kawaida ya kuwashika mkono ndugu zetu wanaokuwa na mahitaji. Tunayatazama makundi maalumu na kuwapa thamani. Tunaamini kwa kwa hili la taulo za kike, walengwa watapata kuwa salama na kurejesha kujiamini.”

Kwa upande wa Mratibu wa kampeni hii ya Buku ya Hedhi Salama, Shufaa Hemed Nasoro amesema kuwa anaishukuru Kampuni ya Meridianbet kuwa mmoja wa wadau wanaokuwa mstari wa mbele kuwasaidia mabinti.

“Nimefurahi sana, nawashukuru Meridianbet kwa mchongo wao. Hili ni jambo jema kwa kuwa tunaenda kuwasaidia mabinti na wanawake ambao wana uhitaji, ili wawe salama wakati wa hedhi, lakini pia kuwapa uwezo wa kujiamini kufanya shughuli zao bila wasi wasi”

Meridianbet ni Kampuni kongwe ya ubashiri wa mtandaoni Tanzania, wakiwa wanatoa huduma za ubashiri wa mtandaoni wa michezo ya kawaida na Kasino ya Mtandaoni.

The post Meridianbet Waunga Mkono Kampeni ya Buku ya Hedhi Salama appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/55138/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT