Skip to main content

MATOKEO MABAYA YANALETA MTIKISIKO

MTIKISIKO unapatikana kila baada ya matokeo mabaya kwenye mioyo ya Watanzania baada ya matokeo mabovu huwa ni mkubwa.

Hili linatokana na namna ambavyo kila mmoja anapenda kuona mafanikio kwa wachezaji wa ndani wanaocheza timu ya taifa.

Haiajalishi ni Timu ya Taifa ya Wanawake, Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars ama timu ya Taifa ya Soka la Ufukweni kikubwa ni matokeo.

Kwa sasa kwa upande wa Timu ya Taifa ya Soka la Ufukweni wapo kwenye maandalizi ya COSAFA ambayo ni mashindano makubwa na muhimu.

Septemba 25-Oktoba Mosi 2022 yanatarajiwa kufanyika haya mashindano huko Durban, Afrika Kusini.

Kikubwa kwa muda huu wa maandalizi mipango muhimu ya ushindi inahitajika na wachezaji kujituma bila kuogopa kwenye msako wa matokeo.

Ukitazama mechi za hivi karibuni timu ya Taifa ya Soka la Ufukweni haikuwa na mwendo mzuri kutokana na kushindwa kupata matoke chanya.

Hata timu ya Taifa ya Wanaume nayo ilikwama kufanya vizuri kwenye mechi za hivi karibuni hapo unaoa kuwa mtikisiko ni mkubwa kwenye mioyo ya Watanzania.

Weka kando hayo kazi inayofuata kwa kila mchezaji ambaye ameitwa kikosi cha timu ya taifa jambo lake ni moja afanye kazi mwanzo mwisho.

Tunawaamini wachezaji mnaweza ila kuaminiwa kwenu kulete majibu ya kweli kwa kila mtakachokifanya uwanjani.

Kila la kheri wachezaji wote mlioitwa kwenye timu na Watanzania wanapenda furaha ambayo inatokana na matokeo mazuri.

Taifa Stars tayari imeshakwea pipa kwa ajili ya mechi mbili za kirafiki ambazo zipo ni dhidi ya Uganda na Libya, kinachohitajika ni maandalizi.

The post MATOKEO MABAYA YANALETA MTIKISIKO appeared first on Saleh Jembe.

The post MATOKEO MABAYA YANALETA MTIKISIKO appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/U7JF0sQ

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT