Skip to main content

Marekani yampongeza Ruto

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Anthony Blinken, amesema katika taarifa kwa vyombo vya habari kwamba anatarajia kwamba ushirikiano kati ya Kenya na Marekani utaimarika chini ya uongozi wa Ruto.

Blinken vile vile amemshukuru mpinzani mkubwa wa Ruto, ambaye ni Raila Odinga kwa kukubali uamuzi wa mahakama.

“Tunampongeza Raila Odinga kwa kukubali uamuzi wa mahakama ya juu. Uchaguzi ulio huru na amani, na hatua ya kufuata mkondo unaofaa kusuluhisha migogoro kupitia kwa taasisi zilizopo ili kukuza demokrasia,” amesema Blinken.

Odinga aliwasilisha kesi mahakamani kupinga ushindi wa Ruto lakini kesi hiyo imetupiliwa mbali kwa kukosa ushahidi.

Ujumbe wa Uingereza

Waziri wa Uingereza anayehusika na maswala ya Afrika Vicky Ford, amesema kwamba Uingereza inatarajiwa kufanya kazi na Dr. William Ruto ili kuimarisha zaidi ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Ford amesema kwamba “Kenya na viongozi wake wameweka mfano mzuri sana kwa ulimwengu kwa jumla kwa kuandaa uchaguzi ulio huru na wazi kabisa.”

Museveni azungumza na Ruto

Rais wa Uganda Yoweri Museveni ameandika ujumbe wa Twitter na kusema kwamba amezungumza na Ruto moja kwa moja na kumtakia kila la heri katika majukumu yake kuiongoza Kenya.

“Nina matumiani mengi kwamba tutashirikiana na Ruto katika kutimiza maslahi ya Jumuiya ya Afrika mMshariki. Mungu aibariki Kenya,” ameandika Museveni.

Ujumbe wa Umoja wa Afrika

Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat amesema kwamba “anampongeza sana rais mteule wa Kenya William Ruto kama rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya na kumpongeza Raila Odinga kwa kuheshimu maamuzi ya mahakama”.

Naye makamu rais wa Ghana Mahamudu Bawumia amesema, “kila la heri kwa rais mteule wa Kenya William Ruto unapochukua uongozi wa taifa la Kenya tunalolipenda. Mungu akuongoze katika kila hatua unayochukua”.

The post Marekani yampongeza Ruto appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/53286/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT