Skip to main content

LUSAJO AIMALIZA RUVU SHOOTING UWANJA WA MAJALIWA


RELLIATS Lusajo ni namba moja kwa utupiaji Bongo akiwa ametupia mabao manne na bao lake la nne aliwatungua Ruvu Shooting, mchezo uliochezwa Uwanjawa Majaliwa.

Kwenye mchezo huo ambao ni wa kwanza kwa Namungo kucheza Uwanja wa Majaliwa msimu wa 2022/23 kutokana na kufanyiwa marekebisho walijitokeza mashabiki wengi na burudani ilikuwa kubwa.

Bao pekee la Lusajo lilifungwa dakika ya 82 zikiwa zimesalia dakika 8 mchezo kukamilika Uwanja wa Majaliwa.

Lusajo anakuwa mzawa wa kwanza kuwa kwenye mwendo wa kufunga kwenye mechi tatu mfululizo kwa kuwa aliwafunga Mtibwa Sugar mabao mawili, Ihefu bao moja na jana kawatungua Ruvu bao moja.

Mwingine ambaye amefanikiwa kutupia mabao kwenye mechi tatu mfululizo ni Moses Phiri wa Simba.

The post LUSAJO AIMALIZA RUVU SHOOTING UWANJA WA MAJALIWA appeared first on Saleh Jembe.

The post LUSAJO AIMALIZA RUVU SHOOTING UWANJA WA MAJALIWA appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/caDOo0h

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT