Skip to main content

Kocha wa Yanga Atumia Dakika 90 Kuwamaliza Al Hilal Ligi ya Mabingwa



Kocha wa Yanga Atumia Dakika 90 Kuwamaliza Al Hilal Ligi ya Mabingwa

Wachezaji wa timu ya Yanga.

KOCHA Mkuu wa Yanga, Mtunisia, Nasreddine Nabi na msaidizi wake, Mrundi, Cedric Kaze, juzi walijifungia ndani kwa dakika 90 na kuungalia mchezo wa hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Al Hilal dhidi ya St George.

Katika mchezo huo uliochezwa nchini Sudan, Al Hilal wakiwa wenyeji walishinda bao 1-0 na kufanikiwa kufuzu hatua ya kwanza ya michuano hiyo ambapo sasa watakwenda kupambana na Yanga kuwania kutinga hatua ya makundi.

Yanga ilikuwa ya kwanza kutinga hatua ya kwanza baada ya kuiondosha Zalan FC kwa jumla ya mabao 9-0, huku mshambuliaji wake, Mkongomani, Fiston Mayele akipiga hat trick mbili katika michezo miwili.

Kocha Mkuu wa Yanga, Mtunisia, Nasreddine Nabi.

Akizungumza na Spoti Xtra, Nabi alisema akiwa na Kaze, waliufuatilia mchezo huo kwa ukaribu na kikubwa kufahamu mbinu, udhaifu wao na wachezaji hatari wa kuchungwa.

Nabi alisema ameona ubora wa Al Hilal ambao ameuficha kwa kukataa kuuweka wazi kwa kuhofia wapinzani kushtuka, zaidi akipanga kukiimarisha zaidi kikosi chake ili kuhakikisha anapata ushindi nyumbani na ugenini.

“Mimi ni kama mwanajeshi, muda wowote nipo tayari kwa ajili ya mapambano, hivyo kukutana na Al Hilal nilitarajia.

“Hivyo kama kocha nimekuwa na utaratibu wa kuwafuatilia wapinzani wangu kwa kuziangalia video za michezo yao ya mwisho waliyocheza kwa ajili ya kuwajua zaidi.

“Wapinzani wetu Al Hilal tayari nimewaona na kuwafahamu wachezaji hatari wa kuchungwa, mbinu na mfumo wanaoutumia, kikubwa ninaendelea kukinoa kikosi changu kitakachopata ushindi,” alisema Nabi.

Yanga itaanzia nyumbani dhidi ya Al Hilal ambapo mechi ya kwanza inatarajiwa kuchezwa kati ya Oktoba 7 na 9, kisha marudiano ni Sudan kati ya Oktoba 14 na 16, mwaka huu.







Toa comment

The post Kocha wa Yanga Atumia Dakika 90 Kuwamaliza Al Hilal Ligi ya Mabingwa appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/wEDOFTf

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT