Skip to main content

Kenyatta akosoa uamuzi wa mahakama wa kutupilia mbali kesi ya Odinga

Katika ujumbe uliorekodiwa na kuwekwa kwenye mtandao wa You Tube, Kenyatta hata hivyo ameonekana kukosoa uamuzi wa mahakama ya juu uliotupilia mbali kesi ya kupinga ushindi wa William Ruto.

Kesi hiyo iliwasilishwa na Raila Odinga wa muungano wa Azimio. Kiongozi mkuu wa muungano wa Azimio ni rais Uhuru Kenyatta.

“Hatua ya kukabidhi madaraka imeanza, ikisimamiwa na kamati iliyoundwa kufanikisha shughuli hiyo, na iliyoanza kazi Agosti tarehe 10. Nia yangu ni kuhakikisha kwamba shughuli ya kupokezana madaraka inafanyika kwa njia nzuri kabisa,” amesema Uhuru.

Hotuba ya Uhuru haijamtaja Ruto wala kumtumia ujumbe wa kheri njema, lakini anataka “wakenya kudadisi zaidi uamuzi wa mahakama ya juu uliotupilia mbali kesi ya Raila Odinga”.

Amedai kwamba “uamuzi wa mahakama haulingani na matarajio ya wakenya kuhusu uchaguzi wa urais na matokeo yake”.

Taasisi za kikatiba zinastahili kujaribiwa

Uhuru amesema kwamba ni “jukumu la kila mkenya kudadisi kwa undani kabisa na kutafuta ukweli kuhusu maamuzi yanayofanywa na taasisi za kikatiba na kuzifanyia majaribio ili kuhakikisha kwamba maamuzi yanayotolewa ni sawa”.

“Je, inahusu hesabu au namna ya kufikia hesabu hiyo? Mchakato huo unafuata kanuni za demokrasia? Je, taasisi inaweza kutoa maamuzi yanayotofautiana kuhusu jambo moja katika mazingira tofauti bila kuchunguzwa?” ameendela kuuliza maswali katika video iliyowekwa kwenye mtandao.

Kenyatta amesema kwamba uamuzi wa mahakama haulingani na uamuzi uliotolewa mwaka 2017, mahakama hiyo ilipofutilia mbali ushindi wake.

Mahakama ya juu ya Kenya ilifutilia mbali ushindi wa Uhuru Kenyatta mwaka 2017 baada ya Raila Odinga kuwasilisha ushahidi kwamba uchaguzi huo ulikumbwa na dosari chungu nzima.

Uhuru Kenyatta amemuunga mkono Raila Odinga katika uchaguzi wa mwaka huu 2022 licha ya ahadi aliyokuwa ametoa kwamba angemuunga mkono naibu wake Dr. William Ruto wakati anapomaliza muda wake wa mihula miwili madarakani.

The post Kenyatta akosoa uamuzi wa mahakama wa kutupilia mbali kesi ya Odinga appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/53284/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT