Skip to main content

ISHU YA KISINDA NA ONYANGO KUJADILIWA TFF


KAMATI ya Sheria na Hadhi za Wachezaji inatarajiwa kukutana Ijumaa kujadili masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na suala la Tusisila Kisinda winga ambaye amesajiliwa Yanga.

Ikumbukwe kwamba Kisinda amesajili Yanga akitokea Klabu ya RS Berkane lakini usajili wake umekwama kukamilika kutokana na usajili wake kuchelewa kwa mujibu wa kanuni ya 62, (1) ya ligi kuu toleo la 2022.

Inaelezwa kuwa kamati hiyo huwa inakutana kwa ajili ya kuweza kujadili masuala mbalimbali ambayo yanakuwa yanawasilishwa mezani.

Ni Said Soud yeye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambayo aliwahi kusema kuwa huwa wanakutana kujadili masuala mbalimbali yanayohusu mpira.

Pia nyota mwingine ambaye anatajwa kujadiliwa ni pamoja na Joash Onyango ambaye anatajwa kwamba amepeleka ombi la kuvunjiwa mkataba na mabosi wake wa Simba..

Ahmed Ally, Meneja wa Habari na Mawasiliano Simba amesema kuwa Onyango ni mchezaji wao na amesaini mkataba wa miaka miwili hivyo bado yupo ndani ya kikosi hicho.

The post ISHU YA KISINDA NA ONYANGO KUJADILIWA TFF appeared first on Saleh Jembe.

The post ISHU YA KISINDA NA ONYANGO KUJADILIWA TFF appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/rV2iFNg

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT