Skip to main content

Zoezi la Sensa laanza kwa mafanikio, waratibu wapewa neno

Na Hadia Khami,s Mtanzania Digital

Kamisaa wa Sensa Spika mstaafu, Anne Makinda amesema zoezi la sensa ya Watu na Makazi 2022 kwa siku ya kuamkia Agost 23, limefanikiwa kwa asimia 17.13.

Akizungumza na waandishi wa habariDar es Salaam Agosti 24, Makinda amesema kiwango hicho kimevuka malengo waliojiwekea kwa siku hiyo kwani walitegemea makarani watafikia asilimia 15.

Amesema zoezi litaendelea kwa muda wa siku saba hivyo ni vyema kwa wananchi kuwa na uvumilivu wa kwamba kila mwananchi ni lazima atahesabiwa.

“Yapo maneno mengi mtaani yanayosemwa kuhusu sensa na wakati mwengine inachanganywa sensa na uchaguzi ninachotaka kusema ni kwamba hii sensa ni siku saba lakini uchaguzi unafanyika siku moja,” amesema Makinda.

Amesema Rais Samia Suluhu Hassan kuitangaza Agost 23, kuwa Siku ya mapumziko ni kuiheshimisha nchi kwa sababu zoezi la sensa ni la umuhimu sanaa linafanyika kwa miaka 10 mara moja.

Aidha, amewataka waratibu wa sensa wa Wilaya na Mikoa kuweka namba maalum ambayo itatumika kwa ajili ya kueka ahadi kwa watu ambao hawaja hesabiwa.

Amesema kupiga cm hizo ni bure hazitakuwa na malipo lengo ni kutaja muda watakaokuwepo nyumbani kwao ili wafuatwe kwa lengo la kukamilisha zoezi.
Amesema vishkwambi vipo vya kutosha hata kama ikitokea vimepotea vipo vya ziada kwa ajili ya kukamilisha zoezi la sensa.

Hata hivyo amewataka viongozi wa serikali za mitaa kuwaongoza makarani wa sensa na kwa kila kiongozi mmoja anatakiwa amuongoze karani mmoja.

“Kwa kila kiongozi atalipwa kulingana na kumuongoza karani wala wasiwe na shaka kwani posho zao zipo,” amesema Makinda.

The post Zoezi la Sensa laanza kwa mafanikio, waratibu wapewa neno appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/50182/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT