Skip to main content

Zoezi la kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa Kenya limehitimishwa rasmi saa 11 kamili jioni hii. Vituo vingi vya kupigia kura …

Zoezi la kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa Kenya limehitimishwa rasmi saa 11 kamili jioni hii.

Vituo vingi vya kupigia kura vilifunguliwa saa 12 asubuhi, ambapo idadi kubwa ya watu wamejitokeza kupiga kura.

Maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Kenya (IEBC)
wamesema, licha ya muda kumalizika, wananchi waliopanga mistari wataendelea kupiga kura mpaka watakapomalizika.

Jumla ya nafasi 1,882 zikiwemo za Urais, Ugavana na Uwakilishi zinagombewa katika uchaguzi huo.

Kwa kiti cha Urais, wagombea wanne wameshiriki katika kinyang’anyiro hicho huku upinzani mkubwa ukiwa kati ya Raila Odinga kutoka muungano wa Azimio la Umoja na William Ruto kutoka muungano wa Kenya Kwanza na Naibu Rais wa nchi hiyo.

Rais Uhuru Kenyatta ambaye anamaliza muda wake alipiga kura katika eneo la Gatundu South na kuwasihi wananchi wapige kura na kurejea majumbani kusubiri matokeo.

Kwenye baadhi ya maeneo kulikuwa na changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja kuchelewa kwa karatasi za kupigia kura ambapo maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Kenya wamesema watafidia muda uliopotea.




Title of the document



The post Zoezi la kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa Kenya limehitimishwa rasmi saa 11 kamili jioni hii. Vituo vingi vya kupigia kura … appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/EcazxHD

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT