Skip to main content

Waumini wa dini waombwa kuendelea kuiombea Nchi

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Waumini wa madhebu ya dini nchini waombwa kuiombea nchi ili kuepukana na majanga mbalimbali likiwemo la njaa, changamoto za kiuchumi zinazo sababishwa ama na binadamu au mataifa mengine, magonjwa, dhiki na mmomonyoko wa maadili.

Waziri George Simbachawene akiteta jambo na Mchungaji Fidelis Mngwabi (katikati) kabla ya ufunguzi rasmi wa sikukuu za vibanda (makambi) za kanisa la waadventista wa Wasabato Magomeni iliyofanyika Kwembe jijini Dar es Salaam.

Wito huo umetolewa leo Jumapili Agosti 14, 2022 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, George Simbachawene wakati wa ufunguzi rasmi wa Sikukuu za vibanda (makambi) za Kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni kwa Mwaka 2022, katika eneo la Kwembe jijini Dar es Salaam yaliyokuwa na Kauli mbiu “NITAKWENDA KWA NGUVU ZA MUNGU”.

“Uwekezaji katika familia imara ni jambo la msingi, bila kwekeza katika familia hakuna nchi hakuna mataifa hakuna dunia. Msukumo wa watu wanaosimamia dhambi kutumia rasilimali fedha kwenye mambo maovu ni mkubwa kuliko msukumo wa kutetea mambo mema,” amesema Simbachawene.

Amefafanua kwamba pamoja na kumtegemea Mungu, bado maandiko matakatifu yanahimiza kufanya kazi kwa bidii.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, George Simbachawene akipokea vitabu kutoka kwa Mchungaji Marko Barnabas, (kushoto) baada ya ufunguzi rasmi wa sikukuu za vibanda (makambi) za kanisa la waadventista wa Sabato Magomeni iliyofanyika Kwembe Jijini Dar es Salaam.

“Katika hili niendelee kuwasihi ndugu Waumini kufanya kazi kwa bidiii huku tukimtumainia Mungu na kuomba baraka zake katika kila kitu. Licha ya kwamba nchi yetu haiegemei upande wowote katika masuala ya dini (Secular State) lakini sehemu kubwa ya watu wake wanaamini katika Mungu kupitia dini na madhehebu mbalimbali.

“Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan inatambuamchango wa Kanisa la Waadventista wa Sabato katika sekta ya elimu kupitia taasisi zake za elimu; sekta ya afya kupitia hospitali na vituo vya afya; pamoja na sekta ya habari kupitia vyombo vya habari vinavyomilikiwa na kuendeshwa na Kanisa.

“Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi na rafiki kwa ustawi wa taasisi hizo ili ziendelee kuwa sehemu ya kuliletea maendeleo Taifa letu,” amesema Simbachawene.

Naye Mchungaji wa kanisa hilo, ambaye pia ni Askofu wa Jimbo la Mashariki Kati mwa Tanzania(ECT), Fidelis Mngwabi katika neno lake la shukrani ameishukuru serikali kwa kutambua mchango wa kanisa la Waadventista Wasabato katika kulinda umoja amani na upendo.

“Kanisa litaendelea kuwa na msimamo wa Mungu katika kusaidia waumini kwenda katika njia iliyo sahihi,” amesema Askofu Mngwabi.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu George Simbachawene akipanda mti baada ya ufunguzi rasmi wa sikukuu za vibanda (makambi) za kanisa la waadventista wa Sabato Magomeni iliyofanyika Kwembe Jijini Dar es Salaam.

The post Waumini wa dini waombwa kuendelea kuiombea Nchi appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/46935/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT