Skip to main content

Wakazi Magomeni Kota wamuangukia Rais Samia

Na Hadia Khamis, Mtanzania Digital

Waliokuwa wakazi wa Magomeni Kota wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kuwasaidia kupata haki zao za msingi ikiwemo kupewa funguo ili waendelee kuishi ndani ya nyumba hizo.

Akizungumza na Mtanzania Digital, mmoja wa wakazi hao, Zamzam Mwalim amesema ni miaka 12 sasa anaishi katika maisha ya tabu kwa ajili ya kupisha ujenzi wa nyumba hizo.

“Mwaka 2011 tulivunjiwa nyumba na tukapewa mikataba wote watu 644 na mikataba hiyo tulipewa na Halmashauri ya Kinondoni kupitia amri ya mahakama iliyothibitisha kuwa sisi ni wakazi halali na wamiliki wa hizi nyumba,” amesema Zamzam.

Amesema baada ya nyumba kukamilika kujengwa katik zoezi la kukabidhiwa funguo watu 61 wameshindwa kupatiwa funguo hadi sasa.

Amesema wapo baadhi ya watu wanaoendelea kuishi katika nyumba hizo ambao hawana mkataba na hawakuwa wakaazi wa Magomeni Kota.

“Tunamuomba rais na viongozi wake kupitia upya suala la uhakiki ili kuweza kupata haki zetu za msingi tunaimani na Rais Samia na anaweza kutusaidia,”amesema Zamzam.

Upande wake Wakili wa wakazi hao wa Magomeni Kota, Twaha Taslima amesema ni vyema kwa wakala wa Majengo(TBA) kutumia busara ya maridhiano kwa kukaa pamoja ili kuweza kulipatia ufumbuzi suala hili.

Amesema kwa mujibu wa TBA inawataka wakazi hao kwenda mahakamani kitu ambacho kinaweza kuendelea kuleta mgongano.

“Kuishtaki taasisi yoyote ya Serikali ni lazima barua yako ipitie kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kwa mujibu wa sheria atatakiwa asitishe eneo kwa kipindi cha miezi mitatu lisifanye kazi,” amesema Taslima.

The post Wakazi Magomeni Kota wamuangukia Rais Samia appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/S8KB6N5

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT