Skip to main content

Wabunge wa DRC wakosolewa kwa kulipwa mishahara ya juu sana

Kupata taarifa sahihi kuhusu kiasi gani wabunge wanapata nchini DRC ni vigumu.

Hata hivyo, Jumanne, kiongozi wa upinzani Martin Fayulu alisema katika taarifa kwamba malipo ya wabunge hao yamefikia hadi dola 21,000 kwa mwezi na ameomba uchunguzi ufanyike juu ya suala hilo.

“Ninaghadhabika sana,” alisema, akionyesha kwamba asilimia 70 ya raia wa Congo wapatao milioni 90 wanaishi na chini ya dola 2 kwa siku.

“Huu ni ufisadi kwa kiwango kikubwa,” aliongeza.

Taarifa hiyo iliibua msururu wa makala katika vyombo vya habari vya Congo Jumatano, pamoja na bunge la taifa lenye wabunge 500 kukanusha rasmi madai hayo.

Mbunge Samuel Mbemba, ambaye anafanya kazi na spika wa bunge hilo, ameiambia AFP kwamba Fayulu alikuwa “anaota” kwa kutoa kauli hiyo.

Hata hivyo, Tresor Kibangula, mchambuzi katika taasisi ya utafiti iitwayo Ebuteli, anakadiria kuwa kiwango hicho cha mshahara wa wabunge ni sahihi.

The post Wabunge wa DRC wakosolewa kwa kulipwa mishahara ya juu sana appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/vx6OPzn

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT