Skip to main content

Ubungo yaanza kudhibiti ukatili

Na Faraja Masinde, Mtanzania Digital

Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam imenza mkakati wa kudhibiti vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto huku ikianza na maeneo hatarishi.

Lengo la mkakati huo ni kuhakikisha kuwa wanadhibiti matukio yote ya ukatili ambapo wataanza na kata nne za Manzese, Mabibo, Mburahati na Makurumla ambazo ndizo zinaongoza kwa matukio ya ukatili ukiwamo wa kijinsia.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Usawa wa Jinsia Tanzania, Msafiri Mariam ambapo amesema kuwa lengo ni kufikia mkoa mzima wa Dar es Salaam.

“Lengo la kuitisha viongozi wa mtaa, watendaji kata, polisi kata, viongozi wa dini na makundi ya kijamii ni kutaka kutoa elimu ya pamoja na kubadilishana uzoezi namna ya kupambana na vitendo vinavyotokea.

“Tumechagua kata hizo nne kwa kuwa ndizo zinaongoza kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia pia kwenda kuwahamasisha watendaji hawa kwenda kuibu vitendo vya ukatili kwa kuunda kamati za mpango mkakati wa serikali wa kutokomeza ukatili(MTAKUWWA),” amesema Msafiri.

Akizungumzia aina ya ukatili unaoongoza Msafiri amesema kuwa ni ukatili wa kingono unaohusisha ubakaji na ulawiti kwa watoto waadogo hasa wa shule ya msingi.

“Kila siku tunakazi ya kuokoa watoto ndiyo maana utaona kwamba kuna maeneo hatarishi ambayo tunayatazama mitaa kama uwanja wa fisi, shidere na manzese ni sehehemu ambazo zimakuwa siyo salama kwa watoto.

“Pia kuna kukithili kwa rushwa ya ngono kwa wafanyakazi wa ndani ambapo kila siku tumekuwa na kazi ya kutoa msaada na ndiyo sababu tumekuja na mkakati huu,” amesema Msafiri.

Awali, Baadhi ya washiriki wa mkutano huo akiwamo Mwenyekiti wa Mtaa wa Chakula Bora, Oddo Ramadhani amesema kuwa elimu inahitajika ili kukomesha ukatili wa kijinsia kwani kumekuwa na matukio mengi yakiwamo ya wanawake kutelekezwa na wenzi wao sambamba na ubakaji.

“Wanawake wanapigwa sana na wanaume zao, lakini pia watoto wa kike wanabakwa sana, hivyo kwa elimu hii tutaenda kuwaelimuisha wananchi na wataelewa madhara yake,” amesema Oddo.

Sheikh wa Kata ya Manzese, Haji Mohamed amesema kuwa ukatili ni kitu kisichokubalina na kinatakiwa kupingwa kwa nguvu zote.

“Elimu hii nitakayoipata hapa nitaenda kuitumia kwenye mawaidha yetu ili kutoa elimu kwa wananchi kujua athari za matendo hayo, kwani tunataka kuwa na jamii salama,” amesema Mohamed.

Upande wake Editha Ibrahim ambaye ni Mtendaji wa Kata ya Mburahati amesema changamotyo kubwa bado ni upande wa wanawake ambao wamekuwa wakikosa ujasiri wa kujitokeza kuripoti matukio ya ukatili jambo ambalo linachovhea kuzalisha jamii isiyo na maadili.

The post Ubungo yaanza kudhibiti ukatili appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/50961/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT