Skip to main content

TRA yajipanga kukusanya Sh trilioni 23 mwaka 2022/23

Na Hadia Khamis, Mtanzania Digital

Katika Mwaka wa Fedha wa 2022/2023 Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imelenga kukusanya Sh trilioni 23.65 ambayo ni sehemu ya Serikali ya Sh trilioni 41.4 ikilinganishwa na Sh trilioni 22.99 katika makusanyo ya Mwaka 2021/22.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam leo Agosti 12, 2022 Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi, Richard Kayombo amesema makusanyo hayo asilimia 99.22 ya Malengo yametokana na maagizo ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Amesema Rais Samia liwaagiza kukusanya mapato kwa weledi na kukaa na walipakodi kutatua changamoto zao ikiwa kuweka mazingira rafiki ya kulipa kodi.

“Mwaka jana tulizidi kuwekeza kwenye Tehama na uanzishwaji wa Mfumo wa kuwasilisha ritani za VAT kieletroniki ambao umeongeza ufanisi nakuondoa Mapungufu na udanganyifu,” amesema Kayombo.

Amesema katika Mwaka huu wa Fedha wa 2022/23 TRA imelenga kutoa elimu kwa watumishi na wafanyabishara nchini juu ya mabadiliko mbalimbali ya sheria za kodi sambamba na tozo pamoja na ada zinazo simamiwa na taasisi hiyo katika kuratibu taratibu za ukusanyaji na usimamiaji wa mapato ya serikali.

“Marekebisho haya ya sheria za kodi yamelenga kusaidia kuongeza kasi ya kufufua uchumi na kuimarisha sekta za uzalishaji kwa ajili ya kuboresha maisha,” amesema Kayombo.

Kayombo amesisitiza kuwa katika mwaka huu wa fedha TRA imelenga kufanyia marekebisho ya sheria ya ushuru wa bidhaa sura 147, sheria ya magari ya kigeni sura 84 sheria ya kodi ya apato sura 332 na sheria ya ongezeko la thamani sura 148.

Ameogeza kuwa sheria zingine ni pamoja na sheria za usimamizi wa kodi sura 438, sheria ya madini sura 123 , sheria usafirishaji bidhaa nje ya nchi sura 196, sheria ya posta na mawasiliano ya kieletroniki sura 306, sheria usimamizi wa forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya 2004 na sheria nyingineza mapato ya siyo ya kodi.

The post TRA yajipanga kukusanya Sh trilioni 23 mwaka 2022/23 appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/46283/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT