Skip to main content

THRDC Zanzibar yaendesha mafunzo ya haki za binadamu kwa maofisa watekelezaji sheria

Na Asha Bani, Mtanzania Digital

MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Zanzibar (THRDC-Zanzibar) unaendesha mafunzo kwa maafisa wa jeshi la polisi, maofisa kutoka ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP) pamoja na maofisa kutoka Chuo cha Mafunzo (Magereza) Zanzibar.

Mafunzo ya siku mbili yameanza leo Augosti 24, katika ukumbi wa Golden Tulip Hotel, Mjini Unguja huku mgeni rasmi akiwa ni Kamishna wa jeshi la polisi Zanzibar, Hamad Khamis Hamad.

Imeelezwa kuwa mafunzo hayo yamelenga kukuza uelewa wa masuala ya haki za binadamu na kuwakumbusha maofisa wa jeshi la polisi, mawakili kutoka katika ofisi ya mwendesha mashtaka mkuu wa serikali pamoja na maofisa wa chuo cha mafunzo (Magereza) kuendelea kufanya kazi kwa kufuata misingi ya haki za binadamu na kujadili changamoto zilizopo hususani za ukatili wa kijinsia pamoja na ukatili wa watoto ili kushauriana namna bora ya kutatua na kuondokana na vhangamoto hizo.

Pia yameandaliwa kutokana na uwepo wa ongezeko la vitendo vya ukatili wa kijinsia visiwani Zanzibar ambapo kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Juni, 2022 jumla ya kesi 487 za udhalilishaji ziliripotiwa, ukilinganisha na kesi 634 za udhalilishaji zilizoripotiwa kwa mwaka 2021, jambo linalopelekea jeshi la polisi pamoja na mamlaka mbali mbali kuhakikisha jitihada za ziada zinafanyika ili kumaliza kabisa changamoto hizo.

Mafunzo haya ni mwendelezo wa juhudi zinazofanywa na mtandao katika kuhakikisha wadau mbali mbali wa haki za binadamu hasa maofisa watekelezaji sheria wanafanya kazi kwa kufuata misingi ya haki za binadamu hasa katika utekelezaji wa majukumu yao pindi wanapohudumia.

The post THRDC Zanzibar yaendesha mafunzo ya haki za binadamu kwa maofisa watekelezaji sheria appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/50180/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT