Skip to main content

Shirika la Human Rights Watch lawashutumu wanajeshi wa Cameroon kwa “mauaji”

Ripoti ya shirika hilo iliwashutumu wanajeshi wa serikali kwa kuwaua takriban watu 10 na kutekeleza unyanyasaji mwingine kati ya Aprili 24 na Juni 12 mwaka huu, wakati wa operesheni za silaha dhidi ya wanaotaka kujitenga katika eneo hilo linalozungumza luhgha ya Kiingereza.

Wanajeshi hao pia wameripotiwa kuteketeza nyumba 12, kuharibu na kupora vituo vya afya, kuwaweka kizuizini kiholela watu 26, na inakisiwa kuwa idadi ya waliotoweka imefikia 17.

Tangu mwaka 2016, wanajeshi wa Cameroon wamekuwa wakishirikisha vikundi mbalimbali vya watu wanaotaka kujitenga wanaoendesha vita vya msituni katika maeneo yenye watu wengi wanaozungumza Kingereza huko Kaskazini-Magharibi na Kusini-Magharibi kwa nia ya kuanzisha taifa lililojitenga la “Ambazonia”.

The post Shirika la Human Rights Watch lawashutumu wanajeshi wa Cameroon kwa “mauaji” appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/PNZihyM

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT