Skip to main content

Putin na viongozi wa Mali wamezungumzia chakula na usalama

Rais wa Russia Vladimir Putin amefanya mazungumzo ya simu na kiongozi wa muda wa Mali Assimi Goita, yaliyoangazia usafirishaji wa chakula, mbolea na mafuta kuelekea Mali.

Goita ameandika ujumbe wa Twiter akisema kwamba wamezungumzia namna Russia inavyoweza kuisaidia Mali kisiasa.

Goita aliingia madarakani kupitia mapinduzi ya kijeshi miaka miwili iliyopita na amekosolewa na mataifa Jirani Pamoja na nchi za magharibi kwa kuchelewa kuandaa uchaguzi mkuu.

Utawala wa Goita vile vile umeshutumiwa kwa ukandamizaji wa haki za kibinadamu na kushirikiana na mamluki wa Russia kupambana na makundi ya wapiganaji wa kiisalamu.

Wakati huo huo, Mali imesema kwamba wanajeshi wake 42 waliuawa katika shambulizi la wapiganaji wa kiislamu lililotokea Jumapili.

Maafisa wamesema kwamba wanajeshi 22 zaidi walijeruhiwa huku wapiganaji 37 wenye uhusiano na kundi la Islamic state waliuawa.

Shambulizi lilitokea katika mji wa Tessit, ulio katika eneo ambalo limekumbwa na mashambulizi ya mara kwa mara, karibu na mpaka wa Mali, Burkina Faso na Niger.

Maafisa wamesema kwamba shambulizi hilo ndilo baya zaidi kuwahi kutokea nchini Mali katika muda wa miaka 10.

Maelfu ya watu wametoroka sehemu hiyo. Watu milioni mbili wametoroka eneo la Sahel kutokana na ukosefu wa usalama.

The post Putin na viongozi wa Mali wamezungumzia chakula na usalama appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/45923/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT