Skip to main content

Mazungumzo ya nguvu za nuclear za Iran kuendelea Tehran

Mazungumzo yatakayofuata yatawahusisha wajumbe wa Marekani na nchi yingine zenye nguvu duniani.

Shirika la habari la serikali ya Iran IRNA, limeripoti kwamba mazungumzo yataendelea na kushirikisha waandalizi wake.

Marekani ilijiondoa kwenye mkataba wa nuclear na Iran mwaka 2018 wakati wa utawala wa rais Donald Trump, na kuiwekea Iran vikwazo vikali vya kiuchumi.

Iran, ambayo inasisitiza kwamba nguvu zake za nuclear ni kwa ajili ya kuzalisha umeme na wala sio kwa kutengeneza silaha, ilijibu kwa kuendelea kusindika nguzu za nuclear kwa kiwango cha juu ya inavyokubaliwa.

Waziri wa mambo ya nje wa Iran Hossein Amirabdollahian amesema kwamba mkataba wa nguvu za nuclear utazingatia na namna Marekani inataka ujadiliwe na itakavyotilia maanani maslahi ya Iran.

Mazungumzo yasiyokuwa ya moja kwa moja kati ya Iran na Marekani kuhusu mkataba wa nguvu za nuclear mwa mwaka 2015, yalianza alhamisi iliyopita, Vienna.

The post Mazungumzo ya nguvu za nuclear za Iran kuendelea Tehran appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/44765/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT